.................................................
Na Dotto Mwaibale, Dodoma
MKUTANO Mkuu wa Mwaka wa Vyombo vya Utangazaji 2026 umeanza rasmi kwa mawasilisho yaliyowasilishwa na wawasilishaji wabobezi katika Ukumbi wa Mikutano wa New Generation Jijini Dodoma huku ukitoa mwanga wa utatuzi wa baadhi ya changamoto zinazoikabili sekta hiyo.
Akifungua mkutano huo Naibu Waziri Wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo Mheshimiwa Hamis Mwinjuma alisema Serikali imesikia na kuzitatua changamoto za muda mrefu ikiwemo kupunguza ada za usajili ili kuwezesha vyombo vingi kuwa na usajili na kutoa Habari zenye tija kwa jamii na Taifa kwa ujumla
Alisema usajili wa blog ada ya kuomba ni Sh. 1O,000 na ada ya mwaka itakuwa Sh. 50,000.
Kwa upande wa Wazalishaji maudhui ya online (You Tuber) ada ni Sh. 100,000 huku ada ya maombi ikiwa ni Sh.20,000.
Miongoni mwa washiriki wa mkutano huo ni vyombo vya utangazaji ambavyo ni televisheni, redio na mitandao ya kijamii.
Mawasilisho yaliyowasilishwa yalikuwa matatu la kwanza likiwa ni Matokeo na Utekelezaji wa Mapendekezo yatokanayo na utafiti wa Huduma za Utangazaji Nchini yaliyo wasilishwa na Mhandisi Andrew Kisaka kutoka TCRA.
Wasilisho la pili lilikuwa ni Fursa na Faida za Uwekezaji wa Teknolojia katika Utangazaji vijijini, lililowasilishwa na Zuhura Selemani ambaye ni Mhadhiri Msaidizi.
Wasilisho la tatu lilihusu Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) na Huduma za Utangazaji wa Redio Vijijini (Uzoefu wa UNESCO), lililowasilishwa na Mhadhiri Dk. Egbert Mkoko kwa niaba ya Nancy Mwaisaka kutoka UNESCO.
Mkutano huo
wa siku mbili ambao umeanza leo Februari 12, 2026 Jijini Dodoma utafikia tamati
kesho Februari 13, 2026 na umeandaliwa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania
(TCRA), na kuwashirikisha wadau mbalimbali wa habari nchini.Mhadhiri Msaidizi Zuhura Selemani akitoa Wasilisho Kuhusu Fursa na Faida za Uwekezaji wa Teknolojia katika Utangazaji
Vijijini.
Washiriki wakiwa kwenye mkutano huo.
Mkutano ukiendelea.
Wadau wa habari wakiwa kwenye mkutano huo.







No comments:
Post a Comment