Kulikuwa na siku niligundua kuwa ukimya unaweza kuumiza kuliko maneno. Mimi na mke wangu tulikuwa tunaishi nyumba moja, tunalala kitanda kimoja, lakini mioyo yetu ilikuwa mbali sana.
Hakukuwa na ugomvi mkubwa, wala kelele kulikuwa na kimya kizito kilichokuwa kikinikandamiza kila siku.
Nilijaribu kuanzisha mazungumzo, lakini kila nilipofungua mdomo nilikuta ukuta.
Macho yake yalikuwa na machozi ambayo hayakumwagika, nami nikabaki na maswali yasiyo na majibu. Ndoa yetu ilianza kukosa mwelekeo, na siku hadi siku matumaini yalizidi kupungua.








No comments:
Post a Comment