Asha aliamini ndoto yake ilikuwa imetimia. Mahari ilikuwa tayari imelipwa. Tarehe ya harusi ilikuwa imepangwa. Nguo zilishonwa. Kadi ziligawiwa. Familia zote mbili zilikuwa zimeanza maandalizi ya mwisho.
Lakini siku saba kabla ya harusi, kila kitu kilibadilika.
Mchumba wake alianza kuwa kimya. Simu hazikujibiwa. Ujumbe ulisomwa bila majibu. Baada ya siku mbili za sintofahamu, ujumbe mfupi uliingia. Alisema hawezi kuendelea na harusi. Hakutoa sababu ya kueleweka.
Ulimwengu wa Asha ulianguka mbele ya macho yake.
Majirani walianza kunongona. Ndugu walijaribu kuficha aibu. Wengine walimlaumu kimya kimya wakisema huenda kuna jambo alifanya. Lakini Asha alijua ndani yake hakukuwa na kosa alilofanya.








No comments:
Post a Comment