Mhadhiri wa Chuo Kikuu chaa Dar es Salaam Dr. Egbert Mkoko akitoa wasilisho katika Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Vyombo vya Utangazaji, lililohusu utafiti utakaofanywa na chuo hicho kwa kushirikiana na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), ili kujua idadi ya watu wanaoangalia maudhui kwenye vyombo vya utangazaji.
....................................
Na Dotto Mwaibale, Dodoma.
CHUO Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) kwa kushirikiana na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), waanza rasmi kufanya utafiti wa hadhira ya wasikilizaji wa radio, watazamaji na wafuatiliaaji wa maudhui ya majukwaa ya kidijitali.
Hayo yamebainishwa na Mhadhiri wa chuo hicho Egbert Mkoko wakati akiwasililisha wasilisho lililohusu utafiti utakaofanywa ili kujua idadi ya watu wanaoangalia maudhui kwenye vyombo vya utangazaji kwenye Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Vyombo vya Utangazaji 2026 ulioandaliwa na TCRA.
Dr. Mkoko alisema utafiti huo utafuata miongozo ya Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) na kuwa utaanza Februari 15, 2026 kwa kuzungumza ana kwa ana na wadau.
Alisema utafiti huo kwa upande wa radio watafanyiwa mahojiano watu 51, televisheni watu 14 na mitandao ya kijamii watu 57.
Alisema vyombo vya habari vitakavyofikiwa ni radio, televisheni, Cable TV na online.
Dr. Mkoko alisema utafiti huo utagusa maeneo mbalimbali kama vile kujua idadi ya watu ambao wanaangalia maudhui kwa wingi na vyombo gani vya utangazaji ambavyo vinapendwa zaidi.
Alitaja mambo mengine ni maudhui gani zaidi yanayopendelewa na watizamaji kati ya ndani na nje ya nchi na namna maudhui yanavyozingatia watu wenye mahitaji maalumu.
Aidha, alitaja jambo lingine kuwa ni watangazaji wa matangazo wanapendelea kuyatoa kwenye vyombo gani na uzingatiaji wa maudhui ya watoto.
Dr. Mkoko alisema mahojiano hayo ya ana kwa ana na makundi
hayo ambayo yataanza Februari 15, 2026 yatafikia tamati Machi 30, 2026.







No comments:
Post a Comment