MBUNGE SINGIDA MJINI YAGI KIARATU AFUTURISHA, ATOA TENDE KATA ZOTE - SINGIDANI BLOG

Habari za Hivi Punde

Post Top Ad

Wednesday, 11 March 2026

MBUNGE SINGIDA MJINI YAGI KIARATU AFUTURISHA, ATOA TENDE KATA ZOTE

Mkuu wa Mkoa wa Singida, Halima Dendego ambaye alikuwa mgeni wa heshima akizungumza katika futari iliyoandaliwa na Mbunge wa Jimbo la Singida mjini Yagi Kiaratu mjini humo.
Mbunge wa Jimbo la Singida mjini Yagi Kiaratu, akizungumza katika hafla hiyo.
....................................

Na Dotto Mwaibale, Singida

MBUNGE wa Jimbo la Singida Mjini, Mhe Yagi Kiaratu ameandaa futari kwa wananchi wa jimbo hilo na kugawa tende katika kata 18 za jimbo hilo.

Akizungumza katika hafla hiyo Kiaratu amewashukuru wananchi pamoja na viongozi mbalimbali  kwa kushiriki katika futari hiyo, huku akisisitiza kutunza amani iliyopo nchini.

Kiaraatu alitumia nafasi hiyo kumshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa fedha nyingi alizozitoa Mkoa wa Singida kwa ajili ya kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Singida Halima Dendego, alimpongeza Kiaratu, kwa kuandaa futari kwa kipindi cha mwezi mtukufu wa ramadhani.

Dendego amesema hatua ya mbunge huyo kuandaa futari inaonesha jinsi alivyo na moyo wa uzalendo na mshikamano miongoni mwa wananchi, huku akisisitiza kuwa maombi yana nafasi kubwa katika kudumisha amani na maendeleo ya taifa
Hafla hiyo ilihudhuriwa na watu mbalimbali, viongozi wa dini huku baadhi yao wakipata nafasi ya kutoa salamu na kumshukuru mbunge huyo kwa kuandaa futari hiyo katika kipindi hiki cha Mwezi Mtukufu wa Ramadhani.
Shekhati wa Mkoa wa Singida, Zeana Said Salumu akizungumza kwenye hafla hiyo.Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Singida, Martha Gwau akizungumza.  Mbunge wa Jimbo la Singida Mjini Yagi Kiaratu akichukua chakula.Mkuu wa Mkoa wa Singida, Halima Dendego, akichukua chakula.
Wakati wa kula chakula ukiendeleaChakula kikiendelea kuchukuliwa. Huyu ndugu upande wa kulia ni kama anasema ' Niongezee kitumbua kama hiki'

Wageni waalikwa wakipata chakula.
Chakula kikichukuliwa.
Sheikh wa Wilaya ya Singida, Issa Simba akizungumza kwenye hafla hiyo.
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Singida, Eliya Digha, akizungumza.
Mbunge wa Jimbo la Itigi na Mjumbe wa Halmashahuri Kuu ya CCM Taifa (NEC), Yohana Msita akizungumza.
Mbunge wa Jimbo la Singida Mjini, Yagi Kiaratu akigawa tende.
Tende zikigawiwa.
Furaha ikitawala wakati wa kukabidhiwa tende.
Ni tabasamu tu wakati wa kupokea tende kutoka kwa Mbunge wa Jimbo la Singida Mjini Yagi Kiaratu

Taarifa hii imeaandaliwa na Dotto Mwaibale simu namba 0754362990.
 

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad