Maumivu ya ndoa yenye usaliti
Neema Mwashighadi, mkazi wa Voi, anasema aliishi katika ndoa yenye huzuni kwa muda mrefu kutokana na tabia ya mume wake kuwa na wanawake wengi. Kwa mujibu wake, hali hiyo ilianza polepole lakini baadaye ikawa ya wazi kiasi kwamba ilianza kuathiri familia nzima.
Alijaribu kumkabili mume wake mara kadhaa lakini hakupata mabadiliko yoyote. Badala yake, mabishano yaliongezeka na nyumbani kukawa na hali ya kutokuelewana kila wakati.








No comments:
Post a Comment