Akizungumza baada ya kukagua daraja hilo, Mheshimiwa Dkt. Mwigulu amesema kuwa ujenzi wa daraja hilo unakwenda kubadilisha historia ya usafiri katika maeneo haya. “Daraja hili limeweka tofauti na lile lililokuwepo awali ambalo halikuwa imara na lilikuwa likisababisha changamoto kwa wananchi na wasafirishaji”.
Ameongeza kuwa Daraja la Sitalike ni sehemu ya miradi ya madaraja inayotekelezwa katika maeneo mbalimbali nchini kwa lengo la kuokoa maisha ya wananchi, kurahisisha usafiri na kuchochea ukuaji wa shughuli za kiuchumi.
Ujenzi wa Daraja hilo ambalo limeshakamilika kwa asilimia 100 limegharimu shilingi bilioni 9.1 na limejengwa na Serikali kupitia Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS).












No comments:
Post a Comment