Kwa muda mrefu nilianza kuota ndoto zile zile karibu kila usiku. Ndoto hizo zilikuwa zinanichanganya sana mara niko sehemu nisiyoijua, mara nakimbizwa, mara naanguka bila mwisho. Nilikuwa naamka nikiwa na hofu na uchovu kana kwamba sikuwa nimelala kabisa.
Mwanzoni nilipuuzia, nikidhani ni mawazo tu ya kawaida.
Lakini kadri siku zilivyopita, ndoto hizo zilianza kurudia kwa mpangilio ule ule. Usingizi wangu ukaanza kuvurugika, na mchana nilikuwa sina nguvu wala utulivu wa akili. Nilijaribu kubadilisha ratiba ya kulala, kupunguza mawazo, na hata kusikiliza ushauri wa watu wa karibu, lakini hali haikubadilika.









No comments:
Post a Comment