Kwa muda mrefu nilikuwa natafuta kazi bila mafanikio. Nilituma maombi sehemu nyingi, nikapitia usaili kadhaa, lakini kila mara nilipata majibu yale yale ya kukataliwa. Ilianza kunitia shaka kuhusu uwezo wangu na hata kujiamini kwangu kulianza kushuka.
Kila siku ilikuwa na matumaini mapya, lakini mwisho wake ulikuwa sawa kimya au ujumbe wa “hujafuzu safari hii.” Ilifika hatua nikaanza kujiuliza kama kuna kitu ninachokosea bila kujua. Nilijaribu kubadilisha CV yangu, kuongeza ujuzi, na hata kuuliza ushauri kwa watu tofauti.









No comments:
Post a Comment