Kulikuwa na mteja niliyefanya naye biashara kwa uaminifu mkubwa. Tulikubaliana bidhaa na malipo yangekamilika ndani ya muda mfupi, lakini baada ya huduma kutolewa, alianza kubadilika. Wiki zikawa miezi. Kila nilipomtafuta, alikuwa na majibu ya kuahirisha mara yuko safarini, mara ana changamoto za kifedha, mara anasubiri malipo mengine yaingie.
Mwanzoni nilikuwa mvumilivu, lakini muda ulivyoenda, hali ilianza kunitia wasiwasi.
Miezi sita ilipita bila malipo yoyote.
Nilihisi kuchoka na kukata tamaa, hasa kwa sababu nilikuwa nimeweka imani yangu yote katika makubaliano yetu. Ilifika hatua nikaanza kuona kama sitawahi kulipwa tena.









No comments:
Post a Comment