𝗠𝗪𝗔𝗡𝗔𝗠𝗞𝗘 𝗔𝗢𝗡𝗗𝗢𝗟𝗘𝗪𝗔 𝗨𝗩𝗜𝗠𝗕𝗘 𝗪𝗔 𝗞𝗜𝗟𝗢 𝟮 𝗠𝗚𝗢𝗡𝗚𝗢𝗡𝗜 𝗕𝗔𝗔𝗗𝗔 𝗬𝗔 𝗠𝗜𝗔𝗞𝗔 𝟭𝟬 - SINGIDANIBLOG

Habari za Hivi Punde

Post Top Ad

Friday, 24 April 2026

𝗠𝗪𝗔𝗡𝗔𝗠𝗞𝗘 𝗔𝗢𝗡𝗗𝗢𝗟𝗘𝗪𝗔 𝗨𝗩𝗜𝗠𝗕𝗘 𝗪𝗔 𝗞𝗜𝗟𝗢 𝟮 𝗠𝗚𝗢𝗡𝗚𝗢𝗡𝗜 𝗕𝗔𝗔𝗗𝗔 𝗬𝗔 𝗠𝗜𝗔𝗞𝗔 𝟭𝟬

Na. Gladys Lukindo- BMH

Daktari Bingwa wa Upasuaji, Sandra Sillas aliye mfanyia upasuaji amesema binti huyo amekuwa akipata maumivu makali yanayo kuja na kupotea.

“Uvimbe huu tuliotoa ulikuwa mgongoni (huge back tumour) ambao una kilo mbili,” alisema Dkt. Sandra.

Ameongeza kuwa kama uvimbe huu usingetolewa ungemletea madhara na ungepelekea saratani.

“Kama uvimbe huu usinge tolewa ungeendelea kukuwa na matokeo yake ungepelekea kuwa saratani, uvumbe huu tulioutoa amekaa nao kwa zaidi ya miaka kumi “ amesema Dkt. Sandra.

Kwa upande wake , mgonjwa huyo aliyefanyiwa upasuaji ameishukuru Hospitali ya Benjamin Mkapa kwa huduma hiyo ya matibabu.

“Nawashukuru madaktari wa Benjamin Mkapa kwa huduma nzuri kabla ya operation nilikuwa siwezi kulala vizuri na hata siwezi kuegemea vizuri lakini sasahvi naendelea vizuri,” ameongeza.

Madaktari Bingwa wa Hospitali ya Benjamin Mkapa wameweka kambi katika hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Manyara ikiwa ni sehemu ya kusogeza na kuhudumia wananchi wenye uhitaji.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad