Kupata mimba ilikuwa ndoto yangu kubwa. Nilifurahi sana mara ya kwanza nilipopata ujauzito, lakini furaha hiyo haikudumu. Nilipoteza mimba bila maelezo ya wazi. Iliniumiza sana, lakini niliambiwa nijaribu tena.
Nilipata mimba ya pili, nikajitahidi kuwa makini zaidi, lakini bado ilipotea tena. Hapo ndipo nilianza kukata tamaa. Nilihangaika sana kutafuta majibu. Nilitembelea hospitali tofauti, nikafanya vipimo vingi, lakini hakuna aliyenipa sababu ya kueleweka.
πKila mtu aliniambia nijaribu tena, lakini moyoni nilikuwa na hofu kubwa. Nilihisi kama kuna kitu kinanizuia kupata mtoto wangu salama.








No comments:
Post a Comment