nilikuwa naishi kwenye familia ambayo haikuwa na amani kabisa. Kila siku kulikuwa na mabishano, maneno makali, na wakati mwingine ukimya mzito uliodumu kwa muda mrefu. Tulijaribu kuzungumza mara kadhaa, lakini kila mazungumzo yaliishia kuwa mabishano makubwa zaidi.
Nilianza kuhisi kama hakuna suluhisho na maisha yetu yangekuwa hivyo kila siku..Hali hii ilinichosha sana. Nilianza kupoteza furaha ya kuwa nyumbani. Hata watoto walikuwa wanaathirika kwa sababu ya mvutano uliokuwa unaendelea kila wakati.








No comments:
Post a Comment