Mtoto wangu alikuwa mzima na mwenye furaha kama watoto wengine. Lakini ghafla alianza kuumwa mara kwa mara bila sababu ya wazi. Wakati mwingine anapata homa, wakati mwingine analalamika maumivu ya mwili, na usiku alianza kuamka akiwa na hofu baada ya kuota ndoto za kuogofya.
Nilimpeleka hospitali mara kadhaa. Vipimo vilifanyika, dawa zikatolewa, lakini hali haikubadilika kwa muda mrefu. Kila alipona kidogo, baada ya siku chache tatizo lilirudi tena. Ilianza kunitia hofu kubwa kama mzazi.








No comments:
Post a Comment