Kila nilipokaribia mitihani, nilikuwa na matumaini makubwa ya kufaulu. Lakini matokeo yalikuwa yale yale kushindwa. Mara ya kwanza nilisema labda sikujitahidi vya kutosha, mara ya pili nikabadilisha mbinu, lakini bado nikashindwa tena. Mara ya tatu ilikuwa mbaya zaidi kwa sababu nilianza kuhisi kama sina uwezo kabisa.
Nilijaribu kusoma kwa bidii zaidi, nikabadilisha mazingira ya kujisomea, na hata kujiunga na vikundi vya masomo. Lakini bado nilihisi kama kuna kitu kinanizuia kuelewa au kukumbuka kile ninachojifunza. Ilianza kunifanya niwe na shaka na uwezo wangu mwenyewe.








No comments:
Post a Comment