Kwa muda mrefu nilikuwa nikimpenda mtu ambaye hakuwahi kuniangalia mara mbili. Kila nilipojaribu kuzungumza naye, nilihisi kama niko mbali sana naye. Nilianza kujiuliza kama kweli nina nafasi yoyote kwake au ni ndoto tu.
Nilijaribu kuwa karibu naye kwa njia za kawaida kuongea, kusaidia pale inapobidi, na hata kujaribu kuonyesha hisia zangu kidogo kidogo.
Lakini bado hakukuwa na mabadiliko. Ilifika hatua nikaanza kukata tamaa kabisa. Nilihisi kama nawapoteza muda wangu na hisia zangu kwa mtu ambaye hanioni hata kidogo. Lakini bado ndani yangu kulikuwa na kitu hakikukubali kuacha kabisa.









No comments:
Post a Comment