Na Claudia Kayombo, Singida
MAHAKIMU 378 wa mahakama za mwanzo nchini wamemwomba
Rais Samia Suluhu Hassan kuwapandisha madaraja.
Miongoni mwa mahakimu hao wapo waliopo kazini kwa
zaidi ya miaka 15 ambao wamekuwa wakisubiri huruma ya serikali ya kupandishwa
madaraja bila mafanikio.
Miongoni mwa mahakimu hao wamebainisha hayo hivi
karibuni huku wakionesha barua iliyoandikwa Oktoba 31, 2018 na kusainiwa na
aliyekuwa kaimu mtendaji mkuu wa mahakama Nyimbi iliyokuwa inakwenda Utumishi
na Utawala bora ikiwaombea kupandishwa madaraja lakini hadi leo hakuna
aliyepandishwa.
Barua hiyo imeainisha kuwa mahakimu wa daraja la
kwanza 198 waliopata cheo cha sasa kuanzia mwaka 2007 hadi 2009 wanaomba kuwa
mahakimu wa mahakama ya mwanzo wakuu nyongeza A huku mahakimu wa mahakama za
mwanzo daraja la kwanza 88 waliopata cheo cha sasa mwaka 2010 wanaomba kuwa
mahakama wa mahakama za mwanzo wakuu daraja la Pili nyongeza B.
Pia mahakimu waandamizi 54 waliopata cheo cha sasa
kuanzia mwaka 2007 hadi 2010 wanaomba kuwa mahakimu wa mwanzo wakuu nyongeza C.
Aidha, mahakimu wa mahakama za mwanzo wakuu 28 waliopata cheo cha sasa mwaka 2007 hadi 2010 wanaomba kuwa mahakimu wa mahakama za mwanzo wakuu I nyongeza D.

.jpg)








No comments:
Post a Comment