WACHUUZI,WANUNUZI SAMAKI WANUSURIKA KIFO. MKOANI LINDI - SINGIDANIBLOG

Habari za Hivi Punde

Post Top Ad

Wednesday, November 29, 2023

WACHUUZI,WANUNUZI SAMAKI WANUSURIKA KIFO. MKOANI LINDI

Mkazi wa Lindi akipita jirani na banda la kuuzia samaki kwa njia ya mnada ambalo limeezuliwa na upepe mkali.

Na Said  Hauni, Lindi.

WACHUUZI wa Samaki wabichi soko la Manispsa ya Lindi,wamenusulika Kifo kufuatia mvua iliyoambatana na upepo mkali kuezua paa la jengo na kudondoshea jengo lingine na kuwaacha watu waliokuwa wanajikinga na mvua kuendelea Kilwa na maji.

Kwa mujibu wa wachuuzi waliokuwepo sokoni hapo,wameeleza mvua iliyoambatana na upepo ilinyesha kwa masaa mawili kuanzia saa nane hadi tisa mchana.

Wakielezea tukio hilo,baadhi ya wachuuzi hao Juma Isumaili,Ashura Ally,Mariamu na Mohamedi Bofu wanasema mvua hiyo imetokea mashariki mwa Bahari ya Hindi kuelekea magharibi.

"Tukiwa tunanadisha samaki upande wa mashariki wingu lilitanda na mvua kunyesha"Wakaeleza wachuuzi hao.

Issa Bakari Bofu akasema wakiwa ndani ya jengo hilo,upepo mkali ulijitokeza na kuezua paa la Banda walimokuwa wamejihifadhi na watu wengine wakiwemo wachuuzi na wanunuzi upepo ukubomoa bati na kupeleka jengo lingine na kuachwa wakiendelea kulowa maji ya mvua.

Alisema licha ya uharibifu huo,hakuna mtu aliyejeruhiwa kwa kukatwa na mabati ya paa hiyo.

Mwenyekiti wa Soko hilo Naibu Abdallah Masera       anakili kuwepo kwa tukio hilo na kueleza anamshukuru mwenyezi mungu hakuna aliyekumbwa na kazia hiyo licha ya uwepo ya idadi kubwa ya watu waliokuwa wamejihifadhi ndani ya banda hilo.

Afisa uvuvi wa Soko hilo, Abdull Twahili amesema upepo huo umesababisha hasara ambayo bado haijaweza kufahamika mara moja hadi hapo wathamini watakapokamilisha kazi yao.

"Kweli hasara ipo tena kubwa tu,kwani yanahitajika bati,boriti na misumali kwa ajili ya utekelezaj wa paa"Alisema Twahili.

Mkurugenzi wa Manispaa Lindi,Juma Mnwele hakuweza kupatikana kuzungumzia mikakati ya matengenezo ya jengo hilo,baada ya kuelezwa yupo safarini.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad