Mbunge wa Viti Maalumu (CCM) Mkoa wa Singida, Aysharose Mattembe (katikati) akigawa vyandarua Hospitali ya Wilaya ya Manyoni wakati wa ziara yake ya kikazi hivi karibuni.
..............................
Na Mwandishi Wetu, Singida
MBUNGE wa Viti Maalumu (CCM) Mkoa wa Singida,
Aysharose Mattembe amefanya ziara ya kikazi kwa kutembelea Hospitali ya Wilaya
ya Manyoni na kukagua ujenzi wa jengo la Mama na Mtoto.
Akizungumza lengo la ziara hiyo Mattembe alisema
ni utekelezaji wa ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ambapo alitembea na
kukagua ujenzi wa jengo hilo na kutoridhishwa na kasi ndogo ya ujenzi.
"Niwaombe kuongeza kasi ya jengo hili la
Mama na Mtoto ili liweze kumalizika haraka na kuanza kutoa huduma ya mama na
mtoto na kuhimarisha afya zao," alisema Mattembe.
Aidha, Mattembe katika ziara hiyo Hospitali hapo
aliweza kugawa vyandarua ambapo aliwataka waliobahatika kugaiwa wakavitumie kwa
ajili ya kuwasaidia kuzuia maambukizi ya malaria na si kwamatumizi mengine.


.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)







No comments:
Post a Comment