Mbunge wa Kilolo, Justine Nyamoga akizungumza wakati wa hafla ya utiaji wa saini ya ujenzi wa mradi wa maji katika Vijiji vya Ng'ang'ange na Mdeke wilayani Kilolo mkoani Iringa............................
Na Mwandishi Wetu, Iringa
Hatimaye kilio cha kero ya maji kiliochokuwa kimewagubika wananchi wa
vijiji vya Ng’ang’ange na Mdeke Jimboni Kilolo kitamalizika baada ya Serikali
kutoa Sh987.7 milioni na kutia saini ya kuanza kwa ujenzi wa mradi huo.
Tayari Wakala wa Maji na Usafi wa
Mazingira Vijijini (RUWASA), Mkoani Iringa na Mkandarasi Africantric
Co. Ltd wametia saini ya mkataba
kwa ajili ya kuanza mradi huo.
Naibu Waziri wa Maji, Mhandisi Kundo Mathew ambaye alikuwa mgeni rasmi
katika hafla ya utiaji saini wa mradi huo amesema lengo la Serikali ni
kuhakikisha wananchi wake wanapata maji
safi na salama.
Mbunge wa Kilolo, Mh Justine Nyamoga ameishukuru Serikali kwa hatua hiyo
kubwa. “Leo mkataba wa ujenzi wa mradi huu umesainiwa, namshukuru sana Rais Dk
Samia Suluhu Hassan, naishukuru Serikali kutukumbuka wana Ng’ang’ange na
Mdeke,”
Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Maji wakiongozwa na Makamu Mwenyekiti wa
Kamati ya Kudumu ya Maji, Mh Anna Lupembe wameshuhudia utiaji huo wa saini.
Viongozi wengine ni wajumbe wa Kamati ya Siasa ya Wilaya ya Kilolo
wakiongozwa na Mwenyekiti wa CCM Wilaya
ya Kilolo, John Kiteve, Madiwani wa Wilaya ya Kilolo wakiongozwa na Mwenyekiti
wa Halmashauri, Anna Msola pamoja na viongozi wa RUWASA.
Mbunge wa Kilolo, Justine Nyamoga akizungumza wakati wa hafla ya utiaji wa
Saini ya ujenzi wa mradi wa maji Ng'ang'ange na Mdeke.
Naibu Waziri wa Maji, Mhandisi Kudo Mathew akizungumza baada ya utiaji wa saini ya ujenzi wa mradi wa maji katika vijiji vya ng'ang'ange na Mdeke Wilayani Kilolo mkoani Iringa.
Wananchi wa Kijiji cha Ng'ang'ange wakiwa kwenye hafla hiyo.








No comments:
Post a Comment