MAHAKAMA ya Wilaya ya Singida imemhukumu aliyekuwa Mkusanya Mapato kwa kutumia mashine ya POS ya Halmashauri ya Manispaa ya Singida, Bw. Kitwana Hamisi Tamba
Mshtakiwa ametiwa hatiani kwa kosa la Matumizi mabaya ya madaraka ambalo ni
kinyume na kifungu cha 31 cha Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Sura ya
329 Marejeo ya Mwaka 2022.
Hukumu hiyo dhidi ya Bw. Kitwana Hamis Tamba katika shauri la Uhujumu
Uchumi Na. 07/2023, imetolewa na Mhe. Fadhil Luvinga - Hakimu Mfawidhi wa
Mahakama ya Wilaya ya Singida - Mei 16, 2024.
Mshtakiwa ameamriwa kulipa faini ya Shilingi 100,000/=, kufidia Jamhuri
Shilingi 500,000/= na kurejesha Tsh 2,043,800/= katika Halmashauri ya Manispaa
ya Singida.
Mshtakiwa huyo alijipatia manufaa ya Shilingi 2,043,800/= kupitia makusanyo ya fedha kwa njia ya POS
ambapo alikuwa akikusanya ushuru katika stendi kuu ya Mabasi Misuna iliyopo
Manispaa ya Singida.
Mshtakiwa amelipa faini na fidia. Pia amerejesha fedha katika Halmashauri
ya Manispaa ya Singida.









No comments:
Post a Comment