Muonekano wa baadhi ya majengo ya Shule ya Msingi Mbezi jijini Dar es Salaam.
.................................
Na Waandishi Wetu, Dar es Salaam
Baadhi ya wazazi na wadau wa elimu katika Manispaa ya Ubungo, kata ya Mbezi
Mwisho wamemtuhumu Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Mbezi na Ufundi, Manispaa ya
Ubungo , kata ya Mbezi kwa ujeuri, kiburi na kugombana na wazazi wa eneo hilo
kuhusu matatizo mbalimbali ya shuleni hapo ikiwamo fedha za masomo ya ziada
(Tuition), gazeti linaripoti.
Akizungumza na waandishi wetu jijini
Dar es Salaam hivi karibuni ambapo hakutaka jina lake litajwe mmoja ya wazazi
alisema kwamba (Jina Kapuni) alisema kwamba Mwalimu Mkuu huyo Daniel Machage ni
mjeuri, kiburi na hana ushirikiano na wazazi kuhusu matatizo mbalimbali shuleni
hapo.
“Kuna kipindi Fulani huko nyuma kwenye kikao cha uongozi wa shule na wazazi
alitaka kupigana hadi kuguchana na mmoja ya wazazi baada ya mzazi kuhoji pesa
ya masomo ya ziada (Tuition),”
“Mmoja ya wazazi aliuliza je kama sina fedha za masomo ya ziada mwanangu
hawezi kuingia darasani alijibu kwa kiburi na dharau ndio wakataka kupigana
mpaka walimu na wazazi wengine wakaingilia kati,’ alisema Mzazi kwa masikitiko
makubwa
Aliongeza kwamba Mwalimu Mkuu huyo hana nidhamu na hataki kushirikiana na
wazazi kwa sababu shuleni hapo kuna tatizo kubwa la maji na watoto wanasoma
bila maji hapo na wakienda kujisaidia hakuna maji kabisa.
Alisema kwamba awali maji yaliwepo shuleni hapo ila Mwalimu huyo mkuu
aliacha kulipa bili za maji akisema kwamba ni kubwa sana na wanafunzi ni wengi
hawezi kuendelea kuingia gharama hizo hata alivyoelezwa kwamba wazazi wapo
tayari kuchangia maji alikataa.
Mzazi huyo aliendelea kusisitiza kwamba pamoja na kiburi na jeuri lakini
hataki kusikiliza maoni ya wazazi ambapo watoto wao wanasoma shuleni hapo,
“Miaka kama mitatu nyuma kuna mtoto aliwahi kufanyiwa vitendo vibaya na
baadhi ya wapiti njia kwa sababu shuleni hapo hakuna ukuta ambapo unaweza
kuwatenganisha wanafunzi na watu wa mitaani,’ alisisitiza
Kwa upande wake mdau mwingine wa
elimu ambaye hakutaka kutajwa alisema kwamba kuna tuhuma za mwalimu mkuu huyo
kwamba anafanyavunyanyasaji kwa walimu hasa wa kike.
Mtoa taarifa mwingine alidai kwamba kuna taarifa zinadai kwamba amekuwa na
tabia ya kukusanya michango kutoka kwa wanafunzi bila kuwa na kikao na wazazi
kama vile mwongozo wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi na Tamisemi
unavyotaka.
Taarifa za awali zilidai kwamba Mwalimu Mkuu huyo ni mbabe ana kiburi ,
anatoa lugha zisizo na staha kwa walimu wa kike na kufanya matendo ambayo ni
kinyume cha maadili kwa viongozi wa umma.
Alipotafutwa na waandishi wa habari hizi , Mkuu huyo wa shule , Bw Machage
alisema kwamba kwamba michango yote kwa ajili ya mitihani ya mihura na moko
inafanywa baada ya kikao cha wazazi kuridhia kama muongozo wa wizara ya elimu
na Mafunzo ya Ufundi unavyotaka.
Bw Machage aliongeza kwamba kila
mwezi wa Juni huwa wanafanya kikao na wazazi shuleni hapo ili kuweza
kujadiliana kwa kina kuhusu matatizo na changamoto za shule na kuweza kutafuta
majawabu kwa pamoja.
“sio kweli mimi nakusanya michanho kwa wanafunzi kupitia wazazi wao bila
kufanya nao vikao huwa tunakuwa na vikao hapa tena safari hii nitawaalika
kwenye kikao cha mwezi wa sita huwa nafunga (Speakers) mpaka kule stendi ya
magufuli wanasikia,” alisema.
Aliongeza kwamba ni kweli fedha kutoka serikalini zinakuja kupitiaTamisemi kiasi cha shilingi
1.2 milioni kila mwezi ila ni kwa ajili ya ukarabati wa shule ,miundombinu ,
vifaa na mambo ya michezo.
Alifafanua kwamba pamoja na mambo
mengine lakini fedha hizi hazitishi na kwa kweli siwezi kukusanya fedha bila
idhini ya wazazi, ,Mkurugenzi na kibali cha Mkuu wa Wilaya (DC).
“Katika hiyo fedha 1.2 millioni utoe
2% ili uweze kugharamia mitihani ya mihura, moko na ya kata kwa wanafunzi
wasipoungua 2,532 na darasa la saba pekee ni wanafunzi 291 hii (capitation)
yaserikali haiwezi kutosha ndugu zangu,”alisisitiza kwa sauti yaupole
Aliendelea kusema kwamba Mkuu wa Wilaya ya Ubungo yaUbungo ingawa hakutoa maandishi ila
yatakuja alisema kwamba kwa madarasa ya mitihani kila wiki wanaweza kuchangia
1500 na kwa madarasa ambayo hayana mitihani kila mwezi 1000.
“Sasa sie hapa tunajibana kwa fedha ya madarasa ambao hawana mitihani ya
kila wiki na tunakusanya kila mwezi na
kugharamia mitihani ya kata kwa sababu hatukusanyi michango kwa ajili ya
mitihani ya kata kutoka kwa wazazi,” alisema kwa kujiamini
Akifafanua juu ya tuhuma hizo alisema kwamba sio kweli kwamba yeye ana
tumia lugha mbaya ni kusimamia kanuni, sheria na taratibu za serikali katika
kuhakikisha taaluma inapanda shuleni hapo,
“Kama mimi ningekuwa na mahusiano
mabaya na walimu wangu nisingeweza kupandisha kiwango cha ufaulu wa shule hii
kwa sababu ufaulu unapanda shule hii ni ya 20 kati 80 katika Wilaya ya Ubungo
tunakwenda vizuri kwa kweli,” aliongeza
Kwa Upande wake, Afisa Elimu wa
Wilaya yaUbungo, Ndugu Denis Nyoni alinukuliwa akisema kwamba michango yote
inayokusanywa shule lazima kuwe kumefanyika vikao kati ta wazazi na uongozi wa
Shule na wazazi kuridhia kuchangia gharama za elimu.
“sikia ndugu yangu fedha za serikali
zinakwenda kila mwezi ila pale am ambapo hapakutosha wanaweza kukusanya
michango kama waraka wa serikali unavyosema na kibali kinatoka kwa Mkuu wa
Wilaya (DC) na si vinginevyi,” alisisitiza Ndugu Nyoni.
Ndugu Nyoni aliongeza kwamba taratibu zote za serikali
zinafuatwa na sio kweli kwamba Mwalimu Mkuu huyo hapo Mbezi anafanya mambo kwa
matakwa yake na mengine watu wanakuwa na maslahi yao kwa kweli ila kama kuna
tofauti naweza kufuatilia.
Kwa Upande Mratibu wa Elimu Kata ya Mbezi, Bi Suzana Massawe alisema kwamba kwa upande wake hajapata malalamiko hayo ya ukusanyaji wa michango kwa ajili mitihani shuleni hapo ila atafuatilia









No comments:
Post a Comment