NSSF YAFANYA MKUTANO MKUU WA BARAZA LA WAFANYAKAZI JIJINI MWANZA - SINGIDANIBLOG

Habari za Hivi Punde

Post Top Ad

Saturday, May 11, 2024

NSSF YAFANYA MKUTANO MKUU WA BARAZA LA WAFANYAKAZI JIJINI MWANZA

Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) Bi.Mwamini Malemi, akizungumza wakati akifungua Mkutano wa 52 wa Baraza Kuu la Wafanyakazi wa NSSF Jijini Mwanza Mei 9, 2024

......................................

Na Mwandishi Wetu, Mwanza 

MWENYEKITI wa Bodi ya Wadhamini ya Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) Bi.Mwamini Malemi, amewataka wafayakazi wa mfuko huo kuboresha huduma bora kwa wnachama wa mfuko huo.

Malemi alitoa maagizo hayo wakati akifungua Mkutano wa 52 wa Baraza Kuu la Wafanyakazi wa NSSF. Jijini Mwanza Mei 9, 2024,

" Boresheni  huduma bora kwa wanachama, wajengeeni uwezo wafanyakazi, ongezeni kasi ya ukuaji wa mfuko kwa kuifikia sekta binafsi na sekta isiyo rasmi na kuimarisha matumizi ya TEHAMA katika utendaji kazi wenu," alisema Malemi.

Aidha, Malemi  alisema NSSF itaendelea kusimamia maono ya Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dkt Samia Suluhu Hassan,  na kuhakikisha Watanzania waliopo katika sekta binafsi na sekta isiyo rasmi wanasajiliwa na mfuko na waajiri wanawasilisha michango stahiki ya wafanyakazi wao kwa wakati.

Alisema lengo la mkutano huo ni kupitia mpango wa mwaka ujao na Bajeti kwa mwaka 2024/25, ikiwa ni ushirikishwaji wa wafanyakazi katika maamuzi ya kiutendaji. 

Mkutano huo ulifanyika Mei 9, 2024 Hoteli ya Malaika Jijini Mwanza.Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), Masha Mshomba, akitoa maelezo ya awali kabla ya ufunguzi wa Mkutano 

 Mkurugenzi wa Usimamizi wa Rasilimali Watu na Utawala wa NSSF, Ekwabi Mujungu, akizungumza kwenye mkutano huo.,
Meneja Uhusiano na Elimu kwa Umma wa NSSF, Lulu Mengele akiratibu ufunguzi wa mkutano huo.
Meneja wa NSSF Mkoa wa Mwanza Emmanuel Kahensa akitoa neno la ukaribisho wakati wa mkutano huo.
Meneja wa NSSF Mkoa wa Kinondoni Large Materu akizungumza kwenye mkutano huo.
Washiriki wakiwa kwenye mkutano huo.
Mkutano ukiendelea.
Mkutano ukiendelea.
Taswira ya mkutano huo.
Viongozi wakiwa meza kuu wakati wa mkutano huo.
Picha ya pamoja na viongozi
Picha ya pamoja.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad