Katibu Mkuu wa TAMUFO Stella Joel
Mlezi wa TAMUFO, Dkt. Frank Richard
.......................
Na Dotto Mwaibale
UMOJA wa Wanamuziki Tanzania (TAMUFO) umeandaa kongamano
la siku moja linalotarajiwa kufanyika Juni 8, 2024 lenye lengo la kuhamasisha maendeleo
mbalimbali.
Katibu Mkuu wa TAMUFO Stella Joel akizungumza na
waandishi wa habari wameona ni vizuri kuandaa kongamano hilo kwa ajili ya
kuwakutanisha wanamuzi kwa ajili ya kujadili maendeleo yao pamoja na kukumbusha
baadhi ya mambo.
“Tumemwalika Apostle Bishop Dastan Maboya kama Mnenaji Mkuu ambaye atatupa neno la Mungu la la kutujenga kuhusu maadili na kuwatia
moyo waimbaji ambao mbao waamejeluhiwa kwa namna moja au nyingine.
Alisema katika hatua nyingine watatumia kongamano
hilo kufanya maombi maalumu ya kuliombea taifa na kuombeana wao kwa kwao.
Kwa upande wake Mlezi wa TAMUFO, Dkt. Frank
Richard alisema katika kongamano hilo watakuwepo viongozi mbalimbali wa
Serikali na taasisi zisizo za Kiserikali ambao watatoa mada na kuwa litafanyikia
Ukumbi wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) Ilala jijini Dar es Salaam.
Dkt. Richard alitumia nafasi hiyo kuwaomba wapenzi wa Muziki wa Injili na wadau wa maendeleo kujitokeza siku ambayo itakuwa na fursa za kimaendeleo zitakazo tolewa na wataalamu waliowaalika na kuwa hakutakuwa na kiingilio chochote.









No comments:
Post a Comment