.................................
Na Dotto Mwaibale, Singidani Blog
MKUU wa Wilaya ya Ikungi Mkoawa Singida, Thomas Apson akishirikiana na
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi, Justice Kijazi wanawaomba Wananchi wa wilaya hiyo kuhudhuria kambi ya matibabu ya Mama
Samia.
Apson ametoa ombi hilo jana alipokuwa
akizungmza na waandishi wa habari kuhusu matibabu yatakayotolewa wakati
wa kambi hiyo ya siku nneitakayoanza kesho kutwa Jumatatu..
"Tunapenda kuwatangazia wananchi wote wa Wilaya ya Ikungi na maeneo ya
jirani kuwa kutakuwa na Kambi ya Matibabu ya Mama Samiaitakayofanyika katika
Hospitali ya Wilaya ya Ikungi iloyopo karibu na ofisi za mkuu wa Wilaya kuanzia
Mei 13, 2024 mpaka Mei 17, 2024,"
alisma Apson.
DC Apson alisma huduma zitakazotolewa ni pamoja na Madaktari Bingwa wa
watoto, Madaktari Bingwa wa wanawake, Madaktari Bingwa wa Upasuaji, Madaktari
Bingwa wa magonjwa ya ndani ikiwemo Figo, Moyo, kisukari na mengineyo,
Madaktari Bingwa wa kinywa na Meno, Tohara kwa watoto na wanaume.
Alisema huduma zote zitatolewa kwa gharama nafuu ambapo alitumia nafasi hiyo kuwakaribisha wananchi wote ili wanufaike na huduma hiyo.









No comments:
Post a Comment