,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,
Na Mwandishi Wetu , Morogoro.
MKUU wa Wilaya ya KIlosa mikoani Morogoro, Shaka Hamdu Shaka amesema kuwa
vyombo vya ulinzi na usalama wilayani humo vinamshikilia Dotto Lusuka (21) huku
vikiendelea kumsaka Suma Lusaka kwa tuhuma za kuhusika na mauaji ya Lazaro
Ndutu, katika Kitongoji cha Kikuyu, Kijiji cha Kigunga, Kata ya Zombo, Tarafa
ya Ulaya.
Akithibitisha kwa vyombo vya habari kuhusu mauaji hayo, Shaka alisema tukio
hilo lilitokea juzi ndani ya hifadhi ya msitu wa kijiji hicho, chanzo ikidsiwa
ni ugomvi uliisababishwa na kuwania eneo msituni humo.
Kwa mujibu wa Shaka ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Usalama ya Wilaya
hiyo, baada ya tukio hilo ndugu walimkimbiza hospitali Ndugu, lakini baadaye
alifariki dunia.
Shaka alisema kuwa Machi mwaka huu, alipokea taarifa za wananchi kuvamia
msitu huo na serikali ikachukua hatua za kupiga marufu uvamizi huo na kufanya
doria kudhibiti vitendo hivyo.
"Ni kweli vyombo vya Ulinzi na Usalama vinamshikilia kijana Dotto Lusuka (Msukuma) miaka 21 kwa tuhuma za kuhusika na mauji hayo ambapo kijana mwingine Suma Lusuka mdogo wa mtuhumiwa aliyekamatwa, naye
anatafutwa na jeshi la polisi baada ya kutoroka..
"Tulipiga marufu na kuimarisha doria katika hifadhi za misituni baada
kupata taarifa za uvamizi na kulielekeza Jeshi la Polisi, TFS na halmashauri
kusimamia matumizi na kulinda hifadhi za misitu
pamoja na juhudi kadhaa kuchukuliwa.
"Licha ya hatua hizo wananchi wamekuwa wakivamia kwa siri na wakati
mwingine kutaka kujichukulia sheria mkononi, kukata miti, kuchoma mkaa na
kufanya uharibifu wa mazingira," alisema Shaka.
Alibainisha kuwa mkakati wa serikali ni kuhakikisha kuwa hifadhi za misitu na rasimali zote muhimu wilayani humo zinaendelea kuwekewa mikakati
madhubuti ili kunusuru athari zaidi za kimazingira na maafa makubwa kuweza kutokea.
"Serikali inalaani vikali mauaji
haya ambayo kimsingi ni kinyume na utu na ubinadamu, kitendo cha kumkata
kata binadamu mwenzio kama nyama ni ukatili uliopotiliza na halitafumbiwa macho
na kwa sasa tunaviachia vyombo vya Ulinzi na Usalama viendele na hatua za
kisheria," alisema.
Alionya tabia ya wananchi kujichukukia sheria mkononi kwa kuwa kufanya
husbabisha madhara mbalimbali ikiwemo vifo na kwamba serikali itamchukulia
hatua kila atakayebainika kuhusika.
Aliwasihi wananchi kutoa taarifa kwa vyombo vya Dola na serikali ya kijiji
kila wanapobaini tatizo lolote ili lishughulikiwe katika njia zilizo sahihi.









No comments:
Post a Comment