Mkuu wa Wilaya ya Urambo mkoani Tabora, Kamishna Msaidizi wa Uhifadhi, Elibariki Bajuta akisisitiza jambo wakati akizungumza na wananchi na viongozi wa AMCOS ya Magulungu hivi karibuni wilayani humo.
.........................
Na Nyamizi Moses, Urambo, Tabora
MKUU wa Wilaya ya Urambo Kamishna Msaidizi wa Uhifadhi, Elibariki Bajuta amewasimamisha kazi na kuwakamata baadhi ya wajumbe na Mwenyekiti wa
bodi ya AMCOS ya Magulungu Kata ya Muungano kwa madai ya ubadhirifu wa fedha za wananchama
wa AMCOS.
Haya yametokea hivi karibuni baada ya Mkuu wa Wilaya kufika katika AMCOS ya
Magulungu ambapo wanachama wa AMCOS wamekuwa wakilalamika kwa muda mrefu
wakidai fedha zao kwa viongozi bila kupata majibu yanayoeleweka kutoka kwa bodi
hiyo.
Katika kikao hicho viongozi wametuhumiwa kwa upotevu wa fedha za wananchama
zaidi ya Sh. Milioni 80 hatua
iliyopelekea Kamishna Bajuta kuagiza kukamatwa kwa viongozi hao na kuagiza
Jeshi la Polisi kuanza uchunguzi kwa kushirikiana na Tasisi ya Kuzuia na
Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) ili kubaini kama kuna upotevu wa fedha hizo
zinazolalamikiwa.
Hata hivyo Kamishna Bajuta amesema serikali haipo tayari kuendelea na baadhi ya Viongozi ambao wanakwamisha maendeleo ya wananchi.















No comments:
Post a Comment