Sheikh wa Mkoa wa Singida, Issa Nasoro akizungumza na Waumini wa Dini ya Kiislamu (hawapo pichani) wakati wa ibada ya Eid Al-Adha iliyofanyika juzi.
........................................
Na Dotto Mwaibale, Singidani Blog.
SHEIKH wa Mkoa wa
Singida, Issa Nasoro amesema Rais Samia Suluhu Hassan kuchangia Sh.Milioni 50
kwa ajili ya ukarabati wa Msikiti wa Taqwa uliopo mjini Singida isiwe nongwa
kwani si mara ya kwanza kwa viongozi mbalimbali kufanya hivyo.
Akitoa hutuba
wakati wa Sikukuu ya Eid Al- Adha iliyofanyika Msikiti wa Taqwa mjini Singida alisema
kuna baadhi ya wanasiasa wameibuka na kudai kuwa eti Rais Samia ametoa hongo
kwa Waislamu wa Mkoa wa Singida kwa kuwapa kiasi hicho cha fedha jambo ambalo
ni kumdhalilisha kiongozi wa nchi.
Sheikh Nasoro
alisema kuchangia michango mbalimbali ya madhehebu ya dini sio mara ya kwanza
amekuwa akifanya hivyo hata katika makanisa sasa anashangaa kuona kwanini
wanasiasa wanalalamikia mchango huo uliotolewa kwa waislamu wa Mkoa wa Singida.
Aidha, Sheikh
Nasoro amewataka waislamu Mkoa wa Singida kutokubali kugawanywa na wanasiasa
kutokana na vyama vyao vya siasa badala yake waendelee kuujenga uislamu wao.
Alisema kuna nchi nyingine
wananchi wake wanashindwa kupata hata muda wa kuabudu kutokana na kukosekana
kwa amani kulikosababishwa na wanasiasa hivyo aliwataka waislamu hasa vijana
kutokubali vishawishi vyovyote ambavyo vinaweza kuhatarisha amani iliyopo
ipotee na badala yake akawaomba vijana kuhakikisha amani hiyo inalindwa na
kudumu na kujikita zaidi kuwalinda viongozi wa nchi.
Akizungumzia kuhusu
iddi ya kuchinja (Eid Al- Adha alisema kila mwislamu anaweza kufanya hivyo akitolea
mfano kuwa Mkoa wa Singida una maeneo makubwa ya ardhi wanaweza wakatengeneza
eneo ambalo kila mwislamu akaweka mbuzi na ngombe kati ya mmoja hadi wawili na
wakati wa chinja unapowadia nao wakaenda kufanya ibada hiyo hata nje ya nchi
kwani jambo hilo lipo ndani ya uwezo wao badala ya kutegemea wageni kutoka
Uturuki na maeneo mengine kuja kuwafanyia.
Sheikh wa Mkoa wa Singida, Issa Nasoro akizizitiza jambo katika swala hiyo.
Sheikh ,Nasoro akiomba dua wakati wa swala hiyo.
Sheikh wa Mkoa wa Singida, Issa Nasoro (kushoto) akiwa na Katibu wa Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA) Mkoa wa Singida wakiwa na mawakala wa uchinjaji wa wanyama wakielekea kukagua zoezi la uchinjaji eneo la Uhamaka lililopo Manispaa ya Singida.
Sheikh wa Mkoa wa Singida, Issa Nasoro akisalimiana na mmoja wa mawakala kutoka Uturuki.








No comments:
Post a Comment