Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora,George Simbachawene ambaye alikuwa mgeni rasmi kwenye Maonesho ya Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma ambayo yamefanyika kitaifa mkoani Dodoma akizungumza na viongozi wa Bohari ya Dawa (MSD) Kanda ya Kati wakati alipotembelea banda lao.
.................................
Na Mwandishi Wetu, Dodoma
VIONGOZI mbalimbali wa Serikali wametembelea Banda la Bohari ya ya Dawa (MSD) kwenye maonesho
ya Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma ambayo yanafanyika kitaifa mkoani Dodoma kuanzia tarehe 16 hadi
23 June, 2024.
Miongoni mwa viongozi waliotembelea ni Mgeni rasmi katika maadhimisho hayo
Mhe. George Simbachawene Waziri wa Nchi,
Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora pamoja na Mhe.
Ridhiwani Kikwete (Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi
wa Umma na Utawala Bora.
Mhe. Simbachawene amesema anafurahishwa na namna MSD inavyotekeleza
majukumu yake katika kuhakikisha upatikanaji wa bidhaa za afya “nimefurahishwa
na namna MSD ilivyosambaza mashuka kwenye majimbo yetu ambayo yamesaidia katika
utoaji wa huduma za afya”
Mhe. Simbachawene ameipongeza pia MSD kwa kupeleka haraka Jokofu la
kuhifadhia miili Kituo cha Afya Kibakwe – Mpwapwa - Dodoma ambalo lilikuwa
linahitajika kwa kiasi kikubwa.







No comments:
Post a Comment