SHEIKH MKOA WA SINGIDA ALIVYO KAGUA UCHINJAJI WANYAMA, EID AL- ADHA ATOA ONYO KWA MAWAKALA - SINGIDANIBLOG

Habari za Hivi Punde

Post Top Ad

Thursday, 20 June 2024

SHEIKH MKOA WA SINGIDA ALIVYO KAGUA UCHINJAJI WANYAMA, EID AL- ADHA ATOA ONYO KWA MAWAKALA

Uchunaji wa ng'ombe ukifanyika katika eneo la Mwaja nje kidogo ya Manispaa ya Singida.

.........................................

Na Dotto Mwaibale, Singidani Blog


Na Dotto Mwaibale, Singida

SHEIKH wa Mkoa wa Singida amemaliza kukagua vituo vilivyotengwa kwa ajili ya zoezi la uchinjaji wa wanyama  wakati wa Sikukuu ya Eid Al- Adha.

Akizungumza na waandishi wa habari baada ya kukagua maeneo yote ya kuchinjia wanyama hao Sheikh Nasoro alizipongeza taasisi zote zilizofanya vizuri kwa uchinjaji.

"Kuna baadhi ya taasisi zimefanya vizuri kwa kufuata maelezo ya Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA) na Serikali kupitia idara ya mifugo ambapo zimechinja wanyama wenye sifa kama dini inavyotaka, kutenga maeneo maalumu ya kuchinjia ambayo yamejengwa kisasa na kuweka ulinzi wa kutosha kuepusha vurugu jambo ambalo kumekuwa na utulivu na wananchi kupata sadaka yao bila ya bugudha," alisema Nasoro.

Sheikh Nasoro alizitaka taasisi ambazo hazikufanya vizuri kuiga taasisi zilizofanya vizuri na kuwa jambo hilo ndio hitaji la walaji wa wanyama hao wa sadaka.

Sheikh Nasoro alitoa wito kwa mawakala wa wajichaji hao kujenga tabia ya kufuata maelekezo yanayotolewa na kununua wanyama waliobora ambao wanalingana na thamani halisi ya hela wanazopewa na wahusika kwa ajili ya kazi hiyo na si vinginevyo na kuacha tabia ya kununua wanyama waliodhoofu kondefu na wagonjwa kwa bei ya chini lengo likiwa ni kujipatia fedha na kuhatarisha afya za walaji wa nyama hiyo.

“Natoa onyo kwa mawakala wote wanaokiuka taratibu na kanuni zilizowekwa kuacha tabia ya kununu wanyama ambao hawana sifa ninawaomba wawe waadilifu vinginevyo hatuta ruhusu wanyama wao kuchinjwa ,” alisema Sheikh Nasoro.

Sheikh wa Mkoa wa Singida, Issa Nasoro akizungumzia Taasisi zilizofanya vizuri wakati wa chinja ya Sikukuu ya Eid Al- Adha.
Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Mwaja, John Pascal akizungumzia zoezi la uchinjaji lilivyofanikiwa katika eneo hilo.
Sheikh wa Mkoa wa Singida, Issa Nasoro akizungumza na askari polisi waliokuwa wanaimarisha  ulinzi eneo la uchinjaji wanyama Mtaa wa Mwaja.
Baadhi ya ng'ombe ambao ni dhoofu wakisubiri kuchinjwa katika moja ya kituo cha kuchinja.
Mmoja wa ng'ombe akiwa na hali mbaya akisubiri kuchinjwa kwa ajili ya kitoweo cha Sikukuu ya Eid Al- Adha.
Ngombe huyo akiwa hoi wakati akisubiri kuchinjwa katika moja ya kituo.
Wanawake wakiondoka na kitoweo chao baada ya kukabidhiwa.
Mmoja ya ng'ombea akiwa amekufa na kutoa harufu kali katika moja la eneo la uchinjaji na kuhatarisha usalama wa afya za wananchi.
Sheikh wa Mkoa wa Singida, Issa Nasoro akizungumza na viongozi wa moja ya taasisi ya uchinja alipowasili katika kituo hicho kukagua shughuli za uchinjaji.
Watoto wa Mtaa wa Mwaja wakisubiri kupata kitoweo wakati wa uchinjaji.
Muonekano wa ng'ombe wenye siha njema waliochinjwa katika moja ya kituo cha uchinjaji eneo la Mwaja.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad