VIJANA KATA YA ITIGI WATAKIWA KUTUMIA FURSA ZILIZOPO KUJIKOMBOA KIMAISHA - SINGIDANIBLOG

Habari za Hivi Punde

Post Top Ad

Friday, June 21, 2024

VIJANA KATA YA ITIGI WATAKIWA KUTUMIA FURSA ZILIZOPO KUJIKOMBOA KIMAISHA

Vijana wa Kata ya Itigi wakifurahia jambo wakati wa kikao kazi kilichofanyika Juni 19, 2024 mkoani Singida

......................

Na Dotto Mwaibale 

VIJANA wa Kata ya Itigi mjini mkoani Singida wametakiwa kufanya kazi kwa bidii na kuzitumia vizuri fursa zilizopo wilayani humo kwa lengo la kujikomboa kiuchumi hasa katika kufanya kilimo na biashara

Ombi hilo limetolewa na Diwani wa Kata hiyo   𝐴𝑙𝑙𝑦 𝑀𝑖𝑛𝑗𝑎 wakati akizungumza na vijana hao katika kikao kazi kilichowakutanisha na wadau mbalimbali kilicho keti Juni 19, 2024 kwa lengo la kuzungumzia fursa  zilizopo kwenye kata hiyo.

"Vijana mna kila sababu ya kuzichangamkia fursa zilizopo kwenye kata yetu hasa ya kilimo na  biashara badala ya kukaa tu mkipoteza muda," alisema Minja.

Pamoja na mambo mengine katika kikao hicho viongozi wa kata hiyo waliweza kutoa elimu kwa vijana hao waliweza kupatiwa elimu ya ujasiriamali na athari za dawa za kulevya kwa kundi hilo.

Kwa upande wake Afisa 𝑀𝑡𝑒𝑛𝑑𝑎𝑗𝑖 wa 𝑘𝑎𝑡𝑎 hiyo, 𝑆𝑎𝑖𝑚𝑜𝑛 𝑆𝑖𝑟𝑖𝑙𝑜, 𝑎𝑙𝑖𝑡𝑜𝑎 𝑒𝑙𝑖𝑚𝑢 𝑦𝑎 𝑢𝑗𝑎𝑠𝑖𝑟𝑖𝑎𝑚ali na kuwasisitiza vijana hao 𝑘𝑢𝑎𝑐ℎ𝑎𝑛𝑎 𝑛𝑎 𝑚𝑎𝑚𝑏𝑜 𝑦𝑎𝑠𝑖𝑦𝑜 𝑛𝑎 𝑡𝑖𝑗𝑎 𝑏𝑎𝑑𝑎𝑙𝑎 𝑦𝑎𝑘𝑒 wafanye kazi kwa bidii ili kuiletea maendeleo kata hiyo.

Naye 𝑃𝑎𝑠𝑐ℎ𝑎𝑙 𝑀𝑎𝑠𝑠𝑒𝑙𝑒, alizungumzia  𝑗𝑢𝑢 𝑦𝑎 𝑎𝑡ℎ𝑎𝑟𝑖 𝑧𝑎 𝑑𝑎𝑤𝑎 z𝑎 𝑘𝑢𝑙𝑒𝑣𝑦𝑎 𝑛𝑎 𝑗𝑖𝑛𝑠𝑖 zitakavyoweza kukatisha ndoto zao za maisha na kujikuta wakishindwa kuinuka kimaisha na kuinua uchumi wa Taifa baada ya kupoteza nguvu kazi.

Kikao kazi hicho kikiendelea.
Watoa mada wakiwa kwenye kikao hicho. Kutoka kushoto ni Paschal Masele, Diwani wa kata hiyo, Ally Minja na Afisa 𝑀𝑡𝑒𝑛𝑑𝑎𝑗𝑖 wa 𝑘𝑎𝑡𝑎 hiyo, 𝑆𝑎𝑖𝑚𝑜𝑛 𝑆𝑖𝑟𝑖𝑙𝑜.
Diwani wa Kata ya Itigi mjini Ally Minja akizungumza kwenye kikao hicho.

Afisa 𝑀𝑡𝑒𝑛𝑑𝑎𝑗𝑖 wa 𝑘𝑎𝑡𝑎 hiyo, 𝑆𝑎𝑖𝑚𝑜𝑛 𝑆𝑖𝑟𝑖𝑙𝑜 akitoa mada kwenye kikao hicho.

Furaha ikitamalaki wakati wa kikao hicho.
Kikao kikiendelea.
 

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad