Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Maliasili kutoka Marekani ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Arkansas, Mhe. Bruce Westernman (kushoto) akimkabidhi zawadi Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Angellah Kairuki (Mb) mara baada ya kikao kati yao kuhusu kushirikiana katika masuala ya uhifadhi, uwindaji wa kitalii na namna ya kuunga juhudi za pamoja katika kupambana na ujangili kilichofanyika katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA)Juni 1,2024. Wanaoshuhudia ni Mkurugenzi wa Idara ya Wanyamapori, Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt. Fortunata Msofe(kulia) na Mwenyekiti wa Bodi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA) (wa pili kutoka kulia).

Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Angellah Kairuki (Mb) akimkabidhi zawadi ya shuka la kimasai Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Maliasili kutoka Marekani ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Arkansas, Mhe. Bruce Westernman (kushoto) mara baada ya kikao kati yao kuhusu kushirikiana katika masuala ya uhifadhi, uwindaji wa kitalii na namna ya kuunga juhudi za pamoja katika kupambana na ujangili kilichofanyika katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA)Juni 1,2024. Anayeshuhudia ni Mwenyekiti wa Bodi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA) (kulia).
Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Angellah Kairuki (Mb) akizungumza na Wawakilishi 11 wa Bunge la Wawakilishi-Congress kutoka nchini Marekani ) kuhusu kushirikiana katika masuala ya uhifadhi, uwindaji wa kitalii na namna ya kuunga juhudi za pamoja katika kupambana na ujangili katika kikao kilichofanyika katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA)Juni 1,2024.

Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Angellah Kairuki (Mb) 9wa sita kutoka kulia) katika picha ya pamoja na Wawakilishi 11 wa Bunge la Wawakilishi-Congress kutoka nchini Marekani ) mara baada ya kikao kati yao kuhusu kushirikiana katika masuala ya uhifadhi, uwindaji wa kitalii na namna ya kuunga juhudi za pamoja katika kupambana na ujangili kilichofanyika katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA)Juni 1,2024. Kushoto kwake bi Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Maliasili kutoka Marekani ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Arkansas, Mhe. Bruce Westernman (kushoto) na wengine ni ni Mkurugenzi wa Idara ya Wanyamapori, Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt. Fortunata Msofe(wa tatu kutoka kushoto) na Mwenyekiti wa Bodi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA) (wa saba kutoka kushoto) na watendaji kutoka Taasisi zilizo chini ya Wizara ya Maliasili na Utalii.
....................................
Na Happiness Shayo
Wawakilishi 11 wa Bunge la
Wawakilishi-Congress kutoka nchini Marekani wameridhishwa na juhudi za uhifadhi
zinazofanywa na Serikali ya Tanzania
huku wakisifia namna ambavyo hifadhi za Taifa zimesheheni wanyamapori.
Hayo yamesemwa katika kikao kati ya
Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Angellah Kairuki (Mb) na Wabunge hao
kilichofanyika katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) Juni
1,2024.
Akizungumza kwa niaba ya Wawakilishi
hao, Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya
Maliasili kutoka Marekani ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Arkansas,
Mhe. Bruce Westernman amesema kuwa wamepata fursa ya kujifunza kuhusu uhifadhi
na kutembelea Hifadhi ya Taifa ya
Serengeti na Eneo la Hifadhi ya Ngorongoro.
" Tumefurahi kujionea
Wanyamapori wengi wakiwemo wanyamapori
watano wakubwa ambao ni kivutio kikubwa cha utalii (big five) ambao ni Simba, Chui, Tembo ,Nyati
na Kifaru" amesema.
Aidha, amesema katika kikao hicho wamepata fursa ya
kujadiliana kuhusu kushirikiana hasa katika masuala ya uhifadhi, uwindaji wa
kitalii na namna ya kuunga juhudi za pamoja katika kupambana na ujangili.
Naye, Waziri wa Maliasili na Utalii,
Mhe. Angellah Kairuki (Mb) amesema kuwa amefurahi kukutana na ujumbe wa Kamati
ya Maliasili kutoka Bunge la Wawakilishi la Congress.
“Tumewashukuru kwa namna ambavyo
wameendelea kutoa ushirikiano na kusaidiana nasi kupitia Shirika la la Marekani
la Maendeleo ya Kimataifa (USAID) katika
jitihada mbalimbali za kuhakikisha tunakuwa na uhifadhi imara endelevu,
harakati mbalimbali za kudhibiti ujangili pamoja na utoaji wa elimu kwa
wananchi kuhusiana na suala zima la uhifadhi na kujua mipaka yao” Waziri
Kairuki amesisitiza.
Vilevile, Mhe. Kairuki ametoa rai kwa
Wabunge hao kuona namna bora ya kuendelea kushirikiana na
taasisi zao hasa katika shughuli za uhifadhi na wanyamapori ili kuweza
kuhakikisha kwamba uhifadhi wa Tanzania
unaendelea kukua kwa ajili ya kizazi cha sasa na kijacho.
Wawakilishi wa Bunge la
Wawakilishi-Congress kutoka nchini Marekani walianza ziara yao nchini Tanzania
Mei 28,2024 na kuihitimisha Mei 31,2024.
Ziara hiyo ilikuwa na lengo la kujifunza kuhusu Uhifadhi
nchini Tanzania.
No comments:
Post a Comment