Mkurugenzi Mkuu wa Bohari ya Dawa (MSD), Bw. Mavere TukaI, akizungumza na Wahariri wa vyombo vya habari (hawapo pichani waliotembelea MSD Kanda ya Kati kujionea shughuli mbalimbali zinazofanywa na taasisi hiyo.
......................................
Na Dotto Mwaibale, Dodoma
BOHARI ya Dawa (MSD) imeendelea kuchanja mbuga baada ya kufanya maboresho
makubwa ya utendaji kazi wake na kuhakikisha bidhaa za afya zinafika kwa wateja
wao kwa wakati.
Mkurugenzi Mkuu wa MSD, Mavere Tukai akizungumza na wahariri wa vyombo vya
habari ambao walikuwa katika ziara ya kutembelea na kujionea shughuli
mbalimbali zinazofanywa na MSD Kanda ya Dodoma na Kanda ya Iringa ambapo
walipata fursa ya kufika Kiwanda cha kuzalisha mipira ya mikono (Groves) cha
Idofi kilichopo Makambako Mkoa wa Njombe alisema wamefanya maboresho makubwa
ambayo wanajivunia.
"Kama mnavyoweza kukumbuka miaka michache iliyopita huduma zetu
tulizokuwa tukizitoa zilikuwa chini ya asilimia
50 lakini tuliendeea kupambana hadi kufikia mwaka 2022/ 2023 tuliweza
kufikia asilimia 71 na tulipofanyiwa ukaguzi tulikuwa tumefika asilimia
76," alisema Tukai.
Alisema mwaka huu hadi kufikia robo ya tatu ya mwaka walikuwa wamefikia
asilimia 84 jambo ambalo kwao limekuwa
la mafanikio na kueleza kwamba licha ya kazi hiyo nzuri wanayoifanya lakini
bado hawajatimiza malengo yao ya kufika asilimia 90.
Tukai alisema kazi nyingine kubwa
waliyoifanya ni kufanya maboresho ya utendaji kazi kwa kuuacha ule wa zamani na
kujikita zaidi kidijitali ambapo wamelazimika kuacha kutumia karatasi.
Alisema kupitia mfumo huo unaoonesha muda mtumishi aliofika kazini, muda
aliofanya kazi na pia unamtathimini mtu muda alioingia na kutoka kazini na kuwa
umesaidia kuchochochea utendaji wa kazi na kwamba wauunda kwa kushirikiana na washauri elekezi .
Alisema maboresho mengine waliyofanya ni kuongeza magari, ujenzi wa maghara
makubwa ya kisasa katika baadhi ya mikoa ili kurahisisha ufikishaji wa bidhaa
hizo za afya kwa walengwa.
Mwanahabari Mgaya Kingoba akizungumza katika kikao hicho cha mafanikio ya MSD katika utendaji wake.













No comments:
Post a Comment