Mkuu wa Wilaya ya Singida,Godwin Gondwe akipokelewa na Meneja Mkazi wa Shirika lisilo la Kiserikali la Kimataifa la KickStart International alipowasili ya kuzindua na kukabidhi pampu za Umwagiliaji za MoneyMaker kwa wakulima wadogo iliyofanyika Kijiji cha Mtipa Manispaa ya Singida, Julai 3, 2024 .......................................
Na Dotto Mwaibale, Singida
SHIRIKA lisilo la Kiserikali la Kimataifa la KickStart International
ambalo limesajiliwa nchini Marekani lenye makao makuu yake jijini Dar es Salaam limeyakutanisha
mashirika mengine ya MEDA, Kampuni ya TAISH na SEMA ya Mkoa wa Singida kwa
lengo la kushirikiana kuwasaidia wanawake katika ufanyaji wa kilimo cha
umwagiliaji kwa kutumia pampu zinazotolewa na shirika hilo za MoneyMaker.
Meneja Mkazi wa shirika hilo Mwaluko Mpangwa akizungumza
na waandishi wa habari Julai 3, 2024 Kijiji cha Mtipa kilichopo Manispaa ya
Singida wakati wa hafla ya kuzindua na kukabidhi pampu za Umwagiliaji za
MoneyMaker alisema kilimo hicho na kutumia pampu hizo ni cha muhimu sana kwani
hakisubiri mpaka mvua iwepo.
Mpangwa alisema dhima ya shirika hilo ni kuwainua
wakulima wadogo kupitia kilimo cha umwagiliaji ambapo wanataka walau kila kaya
iwe na eneo ambalo linamwagiliwa maji kwa mwaka mzima ili mvua zikikoma
kunyesha waendelee na kilimo bila ya kusubiri mvua.
“Vyanzo vya maji kama visima, mabwawa, maziwa na mito
tunavyo hivyo tunawahimiza wakulima wafanye kilimo cha umwagiliaji kama tunavyo
jua kuwa hivi sasa dunia inapita katika changamoto ya tabia nchi na waathirika wakubwa
ni nchi 17 ziliopo zilizopo jangwa la Sahara na Tanzania ikiwepo,” alisema
Mpangwa.
Mkuu wa Wilaya ya Singida,Godwin Gondwe akizungumza kwa
niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Singida alilishukuru shirika hilo kwa kwenda kuendesha
mradi huo mkoani Singida.
Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika
Sustainable Environment Management Action - SEMA
ambalo limeingia ubia wa ushirikiano na shirika hilo, Ivo Manyaku alisema mradi huo umejikita katika maeneo makubwa mawili moja kupitia Kampuni ya Taish Farm ambao wanashughulika upande wa mifugo kuhakikisha ni namna gani watawasaidia wanawake ambao wanafuga mifugo katika kiwango cha chini na kuweza kuboresha kupata maziwa ambayo yatanunuliwa na kampuni hiyo.
“Sisi Sema kutokana na kufanya kazi Mkoa wa Singida tunawakulima wengi ambao tunefanya nao kazi na kufanya nao mawasiliano nao waliopo mbali na Singida na kuweza kuwaunganisha na kampuni ya Taish, MEDA na shirika la KickStart kupata mahitaji ambayo watayahitaji ili kuweza boresha maisha yao kutokana na shughuli za kilimo na ufugaji kwa kutumia kilimo cha umwagiliaji.
Naye Mkurugenzi wa Kampuni ya TAISH Farm, Hassan Rajabu alisema ushiriano uliopo baina ya mashirika hayo umekuwa na tija kubwa katika uboreshaji wa shughuli zao za kuwainua wakulima kiuchumi.
Mratibu wa mradi kutoka shirika la MEDA, Rebeka Rugola alisema shirika hilo linafanya kazi na washirika wao kwa ajili ya kujenga mazingira wezeshi kwa makundi ya wanawake na wajasiriamali.
Mkulima mdogo wa mbogamboga, Victor Elias mkazi wa Mwankoko Manispaa ya Singida akizungumza kwa niaba ya wenzake baada ya kupewa Pampu ya Umwagiliaji ya MneyMaker alilishukuru shirika hilo na kueleza kwamba sasa ataachana uchotaji wa maji kwa kutumia ndoo na badala yake atatumia pampu hiyo aliyopewa na shirika hilo na kuongeza mazao.
















No comments:
Post a Comment