...................
Na Dotto Mwaibale
SHEIKH Mkoa wa Singida, Issa Nasoro amewataka vijana kurejea kwa Mungu na kutoshawishiwa na wanasiasa ili kuharibu amani ya nchi tuliyoachiwa na waasisi wa Taifa la Tanzania.
Akizungumza na Waumini wa dini ya Kiislamu katika swala ya Ijumaa iliyofanyika Julai 4, 2024 Msikiti wa Masjid Noor uliopo Kata ya Misuna Manispaa ya Singida aliwataka vijana hao kutoshawishina na baadhi ya wanasiasa ambao hawaitakii mema nchi yetu.
“Vijana msidanganyike na wanasiasa hao simameni kwenye misingi ya dini bila kuyumbishwa kwani wanataka kuwatumieni hivyo nawaomba ujana wenu utumieni vizuri na si vinginevyo,” alisema Sheikh Nasoro.
Sheikh Nasoro aliwata vijana kuwaheshimu wazazi wao wote wawili na ndipo wanapopata Baraka za Mwenyezi Mungu kupitia wazazi wao hao na kuwa wanaposhindwa kuwaheshimu wanapata chukizo la Mungu na mafanikio yao kufungwa.
Aidha, Sheikh Nasoro aliwataka viongozi kuwa wazalendo na kulitumikia Taifa kwa uaminifu huku wawa na hofu ya Mungu na kuhakikisha wananchi wanapata haki zao.
Akizungumzia kitabu kilichoandikwa na Mufti wa Tanzania Sheikh Abubakar Zuberi Bin Ali kinachoitwa ni Nani wa Kulaumiwa kuhusu Mmomonyoko wa maadili alisema wanaopaswa kulaumiwa ni viongozi wa dini na waumini wao na akasema kila mmoja wao anapaswa kuwa balozi katika kusimamia maadili katika jamii jambo litakaloondoa vitendo vya ushoga, ulawiti na mambo mengine yote ambayo ni chukizo kwa Mwenyezi Mungu.








No comments:
Post a Comment