Na Dotto
Mwaibale, Singida
VIONGOZI
Waandamizi wa Chama cha Skauti Tanzania (TSA) wakutana na Mkurugenzi Mtendaji
wa Manspaa ya Singida wakiwa safarini kuelekea nchini Burundi.
Viongozi hao
waandamizi ni Kamishna Mkuu Msaidizi Utawala Bora, Fredrick Nguma, Kamishna
Mkuu Msaidizi, Maafa na Ubinadamu, Mwalimu Mary Anyitike na maafisa wengine
ambao wameambatana nao katika safari hiyo.
Kamishna
Mkuu Msaidizi, Maafa na Ubinadamu, Mwalimu Mary Anyitike akizungumza kuhusu
safari hiyo alisema wanakwenda nchini Burundi kuiwakilisha nchi katika mkusanyiko
mkubwa wa Skauti Afrika
(JAMBO REE)
“Nchi zote
wanachama wa Skauti Afrika zitakutana na kufanya shughuli mbalimbali zikwemo za
elimu na za Kiskauti na kuwa kusanyiko hilo litakuwa la siku 10 kuanzia Agosti
2, 2024 hadi Agosti 12, 2024 na kuwa
kutoka Tanzania Skauti 30 watakwenda kuwawakilisha wenzao,” alisema Anyitike.
Anyitike
alisema Skauti ni ndugu na popote pale wanapokutana wanakuwa wamoja kwa kila
jambo kama alivyokuwa akifanya muasisi wa Skauti.
Kwa upande
wake Kamishna Mkuu Msaidizi Utawala Bora, Fredrick Nguma alisema wamelazimika
kumtembelea Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Singida, Jeshi Lupembe kwa
kuwa naye ni Skauti Mwenzao hivyo lisingekuwa jambo la busara kupita Singida
bila ya kumuona kamanda mwenza ambapo alitumia nafasi hiyo kumshukuru kwa
mapokezi mazuri aliyowafanyia.
Mkurugenzi wa Manispaa hiyo Jeshi Lupembe aliwashukuru viongozi hao waandamizi wa Skauti kwa kumtembelea ambapo walikumbushana mambo mengi yanayofaywa na Skauti na kueleza kuwa Manispaa ya Singida ina skauti ambao wanafanya vizuri na akawatakia safari njema na ushiriki mzuri katika kusanyiko hilo na kuwa watanzania wanategemea kupata mambo mazuri watakayopta kwenye kusanyiko hilo.
Maafisa wa Skauti kutoka Dar es SalaamHamadi Mtaliya (kushoto) na Erickson Adams wakiwa katika katika mazungumzo na mkurugenzi huyo.
| Skauti hao wakiondoka baada ya kufanya mazungumzo na mkurugenzi huyo. |








No comments:
Post a Comment