WAZEE WASTAAFU WA MAMLAKA YA USALAMA WA USAFIRI WA ANGA WAANZISHA UMOJA WAO - SINGIDANIBLOG

Habari za Hivi Punde

Post Top Ad

Tuesday, July 9, 2024

WAZEE WASTAAFU WA MAMLAKA YA USALAMA WA USAFIRI WA ANGA WAANZISHA UMOJA WAO

 Mwenyekiti wa Umoja wa Waliokuwa Wafanyakazi wa Mamlaka ya  Usalama wa Usafiri  wa Anga Tanzania (USAWA), Margareth Kyarwenda akizungumza mwishoni mwa wiki wakati wa hafla ya kupitisha katiba ya umoja huo., Kushoto ni Mweka Hazina wa umoja huo, Said Ulaya na kulia ni Katibu Msaidizi wa umoja huo,  Aurelia Mushi
Mweka Hazina wa umoja huo,  Said Ulaya akizungumza wakati wa hafla hiyo. 

...................................

Na Kulwa Mwaibale, Dar es Salaam

 

WALIOKUWA Wafanyakazi wa Mamlaka ya  Usalama wa Usafiri  wa Anga Tanzania, wameanzisha umoja wao ambao kwa kifupi unaitwa  (USAWA) 

Akizungumza mwishoni mwa wiki wakati wa hafla ya kupitisha Katiba ya umoja huo iliyojiri Mikwambe,  Kigamboni, Dar es Salaam, Mwenyekiti wa Umoja huo, Margareth Kyarwenda, alisema lengo la kuanzisha umoja huo ni kusaidiana wakati wa shida na raha. 

Aliongeza kuwa, wazo la kuanzisha umoja huo walilipata mwaka 2021 baada ya kuona manufaa ya  kushirikiana katika shida na raha, na hivyo kuwafikishia wazo hilo wengine ambalo walilipokea kwa mikono miwili," alisema Kyarwenda. 

Aliongeza kuwa Mwaka huohuo 2021 wakachagua viongozi wa mpito, ambao Mwenyekiti  akawa yeye, Makamu Mwenyekiti akawa Aspedito Mfugale, Katibu Juda Mkai, Katibu msaidizi Aurelia Mushi na Mtunza Hazina akawa Lawrence Paul. 

Kyarendwa alisema ilipotokea mmoja wao anaumwa, kufiwa, sherehe kama vile harusi, waliendelea kusaidiana. 

Wakiendelea na utaratibu huo, wakaamua kuwa na Umoja ulio rasmi,na hivyo kuandaa Katiba ambayo ilipitishwa Julai 6,2024 baada ya kumalizika kwa mchakato wake. 

"Leo Julai 6 ndiyo tumekutana tena hapa katika mkutano huu wa nne kwa lengo la kupitisha katiba yetu,namshukuru Mwenyezi Mungu wana USAWA wapatao 32 wameshiriki na ni imani yetu hatua itakayofuata itakuwa na mafanikio makubwa," alisema mwenyekiti huyo. 

Kyarwenda ambaye kwa mjibu wa Katiba, alichaguliwa kuwa Mwenyekiti rasmi kwa miaka miwili ijayo, amesema kuwa,umoja wao una hazina kubwa ya wataalam mbalimbali, kwa kutumia uzoefu walionao ambapo baadhi yao wameupata nje ya nchi, wako tayari kutoa ushauri kwa maswala yahusuyo Usalama wa  Usafiri wa Anga wakati wowote watakapohitajika. 

Katibu wa USAWA wa sasa, Aurelia Mushi, akizungumza wakati wa hafla hiyo, aliwapongeza waliotoa wazo la kuanzishwa kwa umoja huo ambao wamesema umewaunganisha tena baada ya kustaafu, na kuwaleta pamoja. 

"Bila umoja huu huenda ingekuwa vigumu kuonana na wastaafu wenzetu kama ndugu yangu Ulimboka Mwakilili  anayeishi huko  Mbeya na Kaka Simon Kimiti yule pale anayeishi  Arusha," alisema katibu huyo. 

Mwakilili alitoa rai kwa wastaafu wenzake kudumisha upendo, mshikamano, kujitoa kwa hali na mali,jambo litakaloufikisha mbali  umoja wao utakaorithiwa na wote watakaofanya kazi katika mamlaka hiyo ya Usalama wa Usafiri wa Anga nchini. 

Aliongeza kuwa, siku za usoni watabuni miradi kwa ajili ya umoja huo ili kupata  kipato kitakachoinua uchumi wao na taifa kwa ujumla. 

Wakati wa hafla hiyo, iliyohudhuriwa na wastaafu kutoka baadhi ya Mikoa, ulifanyika uchaguzi uliowaweka Madarakani viongozi wapya akiwemo pia Mweka Hazina Mteule Said Ulaya. 

Katika tukio hilo la kihistoria, wastaafu watano wenye umri wa miaka 75 na zaidi, ambao ni Steve Mworia,Saltieli Munisi,Lawrence Paul,Aggrey Maeda,Fred Kitangwa, walitunukiwa tuzo mbalimbali

Mmoja wa  Wajumbe wa Umoja huo, Ulimboka Mwakilili, akichangia jambo.
Mmoja wa waanzilishi wa umoja huo, Mzee  Aspedito Mfugale (mwenye kaunda suti) akiwa kwenye hafla hiyo.

Mwenyekiti wa umoja huo, Mwenyekiti wa Umoja huo, Margareth Kyarwenda,  akisisitiza jambo wakati wa hafla hiyo.
Uchaguzi ukifanyika.

Mwenyekiti wa Umoja huo, Margareth Kyarwenda, akimkabidhi zawadi mmoja wa wazee, Stephen Moria aliyefikisha umri wa miaka 75 tangu astaafu. Kushoto ni mmoja wa wanachama wa umoja huo, Brigedia Mstaafu, Moses Shinyambala.
Kura zikihesabiwa baada ya uchaguzi kufanyika
Katibu Msaidizi wa USAWA., Aurelia Mushi, akizungumza wakati wa hafla hiyo


Msimamizi wa uchaguzi Simon Kimiti akizungumza kwenye hafla hiyo.
 

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad