RAIS MHE. DKT. SAMIA SULUHU HASSAN ATEMBELEA MAKUMBUSHO YA VITA VYA MAJIMAJI, SONGEA MKOANI RUVUMA - SINGIDANIBLOG

Habari za Hivi Punde

Post Top Ad

Monday, 23 September 2024

RAIS MHE. DKT. SAMIA SULUHU HASSAN ATEMBELEA MAKUMBUSHO YA VITA VYA MAJIMAJI, SONGEA MKOANI RUVUMA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiweka shada la maua katika kaburi la Chifu Msaidizi wa Wangoni Nduna Songea Mbano ambaye pia alinyongwa na kukatwakichwa na Wajerumani mwaka 1906. Rais Dkt. Samia ameanza ziara ya kikazi mkoani Ruvuma ambapo atakagua miradi mbalimbali ya maendeleo pamoja na kuzungumza na wananchi 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiweka shada la maua katika kaburi la pamoja la Mashujaa wa Vita vya Majimaji walionyongwa na Wajerumani tarehe 27/02/1906 wakati wa Vita hivyo mjini Songea. Rais Dkt. Samia ameanza ziara ya kikazi mkoani Ruvuma ambapo atakagua miradi mbalimbali ya maendeleo pamoja na kuzungumza na wananchi. 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akitoka kwenye moja ya nyumba yautamaduni wa asili ya Wangoni iliyopo katika Makumbusho ya Vita vya Majimaji, Songea mkoani Ruvuma tarehe 23 Septemba, 2024. 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili katika Makumbusho ya Vita vya Majimaji, Songea mkoani Ruvuma tarehe 23 Septemba, 2024. 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwapungia mkono wananchi wakati akielekea Songea mjini wakati wa ziara yake ya kikazi Mkoani Ruvuma tarehe 23 Septemba, 2024. 

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad