KIHENZILE ATUMIA SOKA KUHAMASISHA WANANANCHI KUJIANDIKISHA DAFTARI LA MAKAZI - SINGIDANIBLOG

Habari za Hivi Punde

Post Top Ad

Saturday, October 19, 2024

KIHENZILE ATUMIA SOKA KUHAMASISHA WANANANCHI KUJIANDIKISHA DAFTARI LA MAKAZI

Naibu Waziri wa Uchukuzi na Mbunge wa Mufindi Kusini, David Kihenzile amepata nafasi ya kuzungumza na wanasoka katika kijiji cha Ihowanza, Wilayani Mufindi akiwataka wasisahau kujiandikisha kwenye daftari la makazi.

Kihenzile amekuwa na ziara ya kata kwa kata katika Jimbo lake akihamasisha wananchi kujiandikisha.

Akizungumza na wananchi wa Ihowanza, Kihenzile amesema  "Tunahitaji viongozi Bora na wachapakazi kuanzia ngazi ya Vijiji, Vitongoji na Mitaa hivyo basi tunapaswa kujiandikisha mapema kwenye daftari la mkaazi ili tuweze kupata nafasi hiyo ya kushiriki katika uchaguzi wa Serikali za mitaa hapo Novemba 27," amesema.

Mbali na mambo mengine Kihenzile amempongeza juhudi kubwa za kuibua vipaji kupitia mabonanza yenye ujumbe mahususi wenye kuhamasisha uchaguzi wa Serikali za mitaa.

Aidha amewataka Wananchi hao kuendelea kumuombea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassani pindi anapotekeleza majukumu yake kwa maslahi mapana ya Wananchi wa Kata hiyo na Jimbo kwa ujumla.

Hivi karibuni Kihenzile alifanya bonanza kubwa katika bonde la Mgololo lililojumuisha Kata zote tatu ikiwemo Kiyowela, Idete na Makungu na kugawa zawadi nono na vifaa mbali mbali vya michezo kwa washindi.

Naibu Waziri wa Uchukuzi na Mbunge wa Mufindi Kusini, David Kihenzile (katikati) akiwa na wanamichezo wa jimbo lake na wanannchi wakati wa uhamasishaji wa kujiandikisha kwa kutumia soka.


 Naibu Waziri wa Uchukuzi na Mbunge wa Mufindi Kusini, David Kihenzile akizungumza na wananchi wa jimbo lake kupitia michezo wakati wa uhamasishaji huo.

Naibu Waziri wa Uchukuzi na Mbunge wa Mufindi Kusini, David Kihenzile amepata nafasi ya kuzungumza na wanasoka katika kijiji cha Ihowanza, Wilayani Mufindi akiwataka wasisahau kujiandikisha kwenye daftari la makazi.

Kihenzile amekuwa na ziara ya kata kwa kata katika Jimbo lake akihamasisha wananchi kujiandikisha.

Akizungumza na wananchi wa Ihowanza, Kihenzile amesema  "Tunahitaji viongozi Bora na wachapakazi kuanzia ngazi ya Vijiji, Vitongoji na Mitaa hivyo basi tunapaswa kujiandikisha mapema kwenye daftari la mkaazi ili tuweze kupata nafasi hiyo ya kushiriki katika uchaguzi wa Serikali za mitaa hapo Novemba 27," amesema.

Mbali na mambo mengine Kihenzile amempongeza juhudi kubwa za kuibua vipaji kupitia mabonanza yenye ujumbe mahususi wenye kuhamasisha uchaguzi wa Serikali za mitaa.

Aidha amewataka Wananchi hao kuendelea kumuombea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassani pindi anapotekeleza majukumu yake kwa maslahi mapana ya Wananchi wa Kata hiyo na Jimbo kwa ujumla.

Hivi karibuni Kihenzile alifanya bonanza kubwa katika bonde la Mgololo lililojumuisha Kata zote tatu ikiwemo Kiyowela, Idete na Makungu na kugawa zawadi nono na vifaa mbali mbali vya michezo kwa washindi.

Naibu Waziri wa Uchukuzi na Mbunge wa Mufindi Kusini, David Kihenzile (katikati) akiwa na wanamichezo wa jimbo lake na wanannchi wakati wa uhamasishaji wa kujiandikisha kwa kutumia soka.


 Naibu Waziri wa Uchukuzi na Mbunge wa Mufindi Kusini, David Kihenzile akizungumza na wananchi wa jimbo lake kupitia michezo wakati wa uhamasishaji huo.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad