Mkuu wa Wilaya ya Temeke Mhe.Sixtus Mapunda akiambatana na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Temeke Ndg. Jomaary Satura leo Februari 22, 2025 wameketi pamoja na Wafanyabiashara wa Temeke ikiwemo Viongozi wao kwa ngazi ya Wilaya, Mkoa na Taifa lengo likiwa ni kusikiliza changamoto zao na kuzipatia utatuzi.
Mkutano huo uliobeba pia Agenda ya kukumbushana na kusisitizana umuhimu wa kulipa Kodi Stahiki kwa wakati ili kurahisisha jukumu la Serikali katika kuwaleta Wananchi Maendeleo umefanyika katika Viwanja vya CCM Temeke Mwisho ukihudhuriwa pia na wataalamu kutoka Manispaa ya Temeke.









No comments:
Post a Comment