.................................................
Na Dotto Mwaibale, Singida
VIONGOZI mbalimbali wa Kata ya Itigi Mjini wamekutana na
vikundi kadhaa vya wanawake wa kata hiyo kwa ajili ya maandalizi ya maadhimisho ya siku ya wanawake
duniani yatakayo fanyika March 5, 2025
kwa ngazi ya Halmashauri.
Viongozi hao waliokutana na vikundi hivyo ni Diwani wa Kata
ya Itigi Mjini Mhe.Ally Minja, Afisa Mtendaji wa kata hiyo, Saimoni Sirilo na Mbuva Mwenda (Cdo)
Diwani wa Kata hiyo Ally Minja akizungumza na waandishi wa
habari alisema wameamua kukutana na kundi hilo kwa lengo la kujadili mambo
kadhaa ikiwa ni maandalizi ya maadhimisho ya siku yao hiyo ambayo yatafanyika
duniani kote.
“ Kama viongozi wa kata hii na umuhimu wa maadhimisho hayo licha
ya kuwa sio siku yetu tumeona ni vizuri tukutane nao tuweze kupanga mambo
kadhaa ikiwa ni maandalizi kuelekea maadhimisho hayo ambayo yataambata na
shughuli mbalimbali za kundi hilo la wanawake ambapo pia kutakuwa na maonyesho
ya bidhaa zao,” alisema Minja.
Mwezeshaji maarufu wa ujasiriamali kwa wanawake hao na
makundi mengine katika wilaya hiyo na Mkoa wa Singida kwa ujumla, Saimoni
Sirilo alisema dhamira yao ni kuendelea kuwajengea uwezo na kuwapa mafunzo ya
utengenezaji wa bidhaa bora na nzuri ili waweze kuibuka washindi katika
maonesho hayo.









No comments:
Post a Comment