Mwenyekiti wa Shirikisho la Vyama vya Watu wenye Ulemavu Mkoa wa Dar es Salaam, Charles Matemba, akizngumza katika mkutano na waandishi wa habari Machi 24, 2025 Makao Makuu ya Chama cha Walemavu Tanzania (CHAWATA) Buguruni Jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mwenyekiti wa Chawata, Wilaya ya Ubungo, Athumani Sembe.
....................................
Na Dotto
Mwaibale, Dar es Salaam
CHAMA cha
Walemavu Tanzania (CHAWATA) Mkoa wa Dar es Salaam kimempongeza Rais wa Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuboresha huduma za walemavu
ikiwemo mkopo wanaokopeshwa kuanzia mtu mmoja.
Akizungumza
na waandishi wa habari Machi 24, 2025, Mwenyekiti wa Shirikisho la Vyama vya Watu wenye Ulemavu
Mkoa wa Dar es Salaam, Charles Matemba alisema Rais Samia amewaboreshea huduma
ukiwemo ushirikishwaji katika masuala mbalimbali.
“ Katika
kipindi hiki cha miaka minne ya uongozi wake walemavu tumekuwa tukipata fursa
za kushiriki semina na kuhudhuria makongamo na hasa kushirikishwa kwenye
mchakato mzima wa uchaguzi jambo ambalo ni kubwa na la heshima kwetu,” alisema
Matemba.
Akielezea
baadhi ya changamoto walizonazo ni kukosekana kwa vifaa saidizi kwa kundi hilo
ambapo ameomba Serikali kulifanyia kazi jambo hilo na kuomba ushirikishwa zaidi
katika masuala ya maamuzi.
Mwenyekiti
wa Chawata, Wilaya ya Kinondoni , Subira Semsimbazi akizungumzia suala la
mikopo ya asilimia nne kwa kundi lao aliishukuru Serikali kwa mikopo hiyo
ambayo imekuwa ikiwasaidia kukuza mitaji yao ya biashara na akatoa ushauri kwa
wanawake wenzao kuitumia vizuri.
Kwa upande
wake Mwenyekiti wa Chawata, Wilaya ya Ubungo, Athumani Sembe alisema changamoto
kubwa waliyonayo hawana ofisi zaidi ya kuahidiwa tu na kuelezea kuwa wanawake
wenye watoto wenye ulemavu wasaidiwe na Serikali.
Mwakilishi wa
vijana wenye ulemavu, Furaha Khalid alisisitiza kutolewa kwa elimu ya fedha kwa
vijana kabla ya kupatiwa mikopo na kuwa semina hizo zitolewe mara kwa mara na
si pale tu wanapokopeshwa.
Naye Katibu
wa Chawata Wilaya ya Kinondoni, Said Machaku aliwaomba waliokopo mikopo hiyo
waweze kuirudisha na akaomba utaratibu wa kukopesha bajaji moja watu watano
kuwa hauna afya kwa wakopaji hivyo aliomba babaji moja ikopeshwe mtu mmoja ili
mkopo huo uweze kuwa na tija kwa muhusika.
Katibu wa Chawata, Wilaya ya Ubungo, Athumani Lubandame alisema mkopo huo wa asilimia mbili wanapaswa wakopeshwaji wapatiwe semina na kusisitiza mkopo huo apewe mtu husika baada ya kufundishwa stadi za uzalishaji.
Mwenyekiti wa Chawata, Wilaya ya Kinondoni , Subira Semsimbazi, akizungumza kwenye mkutano huo na waandishi wa habari.
Katibu wa Chawata, Wilaya ya Ubungo, Athumani Lubandame, akichangia jambo kwenye mkutano huo. Kulia ni Mwenyekiti wa Chawata, Wilaya ya Ubungo, Athumani Sembe.
Mkutano huo ukiendelea. Kutoka kushoto ni Mwenyekiti wa Chawata, Wilaya ya Kinondoni , Subira Semsimbazi, Katibu wa chama hicho Kinondoni, Saidi Machaku na Mtunza Hazina wa chama hicho Mkoa wa Dar es Salaam, Furaha KhalidiMkutano ukiendelea.
Viongozi mbalimbali wa Chawata wakiwa kwenye mkutano huo.











No comments:
Post a Comment