Mtoto Aden Ernest Mlay (17) Mwenye Ulemavu akiwa nyumbani kwao Mtaa wa Muheza Kibaha mkoani Pwani.
................................................
Na Dotto Mwaibale, Dar es Salaam
NGUGU zangu watanzania mwenzenu nimekwama sina mbele wala
nyuma, sina mahala pa kuishi, sina uhakika wa chakula na mtoto wangu ni mlemavu na pia ni mgonjwa,
gharama za matibabu yake ni kubwa sasa ni zaidi ya miezi sita hajaenda shule.
Hivyo ndivyo anavyoanza kujieleza Bi. Naemi Mandimbula (50)
Mkazi wa Mtaa wa Muheza Kibaha mkoani Pwani, mama wa mtoto huyo mwenye ulemavu kuhusu
madhira anayopata kutokana na changamoto mbalimbali za maisha zinazo mkabili
ikiwemo hiyo ya kuumwa kwa mtoto wake Aden Ernest Mlay (17)
“Nimeangaika sana ili nipate msamaha wa matibabu ya mtoto
wangu bado sijafanikiwa siwezi kufanya chochote wala kwenda mbali na nyumbani
kutafuta riziki kwa sababu ya mwanangu jambo ambalo limeongeza ugumu wa maisha
yangu.,” alisema Mandimbula.
Alisema mume wake alimkataa mtoto huyo (Dotto) kwa madai
kuwa katika familia yao huwa hawazai wenye ulemavu na kuwa Kulwa wake yupo
kidato cha tatu wakati ndugu yake huyo akiwa darasa la tano kutokana na changamoto aliyonayo.
Mama huyo anasema mtoto wake huyo ni mlemavu ambaye hawezi
kufanya chochote bila ya kusaidiwa na pia anachangamoto ya maradhi ya ubongo na
kukakamaa mwili na alipokwenda Hospitali aliandikiwa dawa ambazo dozi yake ni
kuanzia Sh. 50,000 hadi 60,000 ambazo anazitumia kwa mwezi fedha ambayo
ameshindwa kuimudu.
Amesema changamoto kubwa aliyonayo ni sehemu ya kuishi baada
ya nyumba aliyokuwa amesitiriwa kuishi kubomolewa kutokana na kujengwa eneo
la Serikali na kuwa hivi sasa anaishi kwenye kibanda alicho jenga kwa muda
kilichopo eneo hilo.
Mjumbe wa shina namba 10 wa Mtaa wa Muheza, Abuu Raphael
amethibitisha kumfahama mama huyo na madhira yote anayoyapitia na kueleza kuwa
amekuwa akimsaidia katika hatua mbalimbali za matibabu ya mtoto huyo huku kubwa
akiomba asaidiwe kupata msamaha wa matibabu na eneo la kuishi kwa kuzingatia
kuwa ni mmoja wa watu waliopo kwenye kundi la kaya maskini.
“Nimekuwa nikimuandikia barua mbalimbali kwenda maeneo
tofauti kwa ajili ya kupata msaada hadi kwa
mkuu wa wilaya amekwisha fika,” alisema Raphael.
Ngugu watanzania mmemsikia huyo mama akielezea changamoto
aliyonayo hivyo anapiga magoti mbele yenu akihitaji msaada wenu iwe fedha na
ushauri kama alivyosema ana mtoto ambaye ni mgonjwa, hana sehemu ya kuishi na
hata kula yake ni ya kubahatisha hivyo shime tujitokeze kumsaidia hata kama
utakuwa na Sh. 1000 kwake ni kubwa kwani kutoa ni moyo wala sio utajiri,
Mtoto Aden Ernest Mlay (17) Mwenye Ulemavu akiwa amepakatwa na mtoto mwezake.
Bi. Naemi Mandimbula (50) Mkazi wa Mtaa wa Muheza Kibaha mkoani Pwani, mama wa mtoto huyo akiwa amempakata mtoto wake, Aden Mlay (17)
Hiki ni kibanda anachoishi BiNaemi Mandimbula (50) na familia yake.












No comments:
Post a Comment