TARURA YATOA SEMINA KWA JUMUIYA YA WANAHABARI MITANDAO YA KIJAMII TANZANIA, (JUMIKITA) - SINGIDANIBLOG

Habari za Hivi Punde

Post Top Ad

Friday, 28 March 2025

TARURA YATOA SEMINA KWA JUMUIYA YA WANAHABARI MITANDAO YA KIJAMII TANZANIA, (JUMIKITA)

Mwakilishi wa Mtendaji Mkuu wa TARURA, Mhandisi Ismail Mafita akifungua  semina hiyo Machi 28, 2025. jJijini Dar es Salaam.

.........................................

Dotto Mwaibale na Angelina Mganga, Dar es Salaam

WAKALA wa Barabara Vijijini na Mijini Tanzania (TARURA) imeandaa semina maalumu kwa ajili ya kuwajengea uwezo  Jumuiya ya wanahabari mitandao ya kijamii Tanzania (JUMIKITA) ili waweze kujua shughuli mbalimbali zinazofanywa na Tarura na kuziandika kwa ufasaha kwa manufaa ya wananchi na Taifa kwa ujumla.

Moja ya mada kubwa ambayo itatolewa katika semina hiyo ni ujenzi wa madaraja kwa kutumia teknolojia ya mawe ambayo ni nzuri na inatunza mazingira mada ambayo itatolewa na Mratibu Ujenzi wa madaraja na barabara za mawe Mhandisi Pharles Ngeleja.

Mada ya pili katika semina hiyo itahusu Uhifadhi wa barabara na mitaro sio jalala ambayo iliwezeshwa na Dkt. Makene Madoshi.

Dkt. Makene Madoshi akitoa mada kwenye semina hiyo

Mratibu Ujenzi wa madaraja na barabara za mawe Mhandisi Pharles Ngeleja. akitoa mada kwenye semina hiyo.
Kaimu Meneja Mahusiano na Mawasiliano TARURA, Catherene Sungura akizungumza kwenye semina hiyo.
Wanahabari wakiwa kwenye semina hiyo.
 

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad