.......................................
Na Solomon Philemon, Singida
WAISLAMU
Singida kusherehekea Sikukuu ya Eid
al-Fitr viwanja vya Bombadia ambapo swala ya iddi
itafanyika hapo pamoja na mambo mengine.
Hayo
yamebainishwa na Sheikh wa Mkoa wa Singida, Issa Nasoro wakati akizungumza
katika mkutano na waandishi wa habari ofisini kwake Machi 29, 2025 mjini
Singida.
“ Niwasihi
Waislam wote wa Manispaa ya Singida mfike mapema kwenye viwanja hivyo kwa ajili
ya swala ya iddi ambayo itafanyika saa tatu kamili na baada ya hapo watu
watatawanyika kwenda kusherehekea sikukuu hiyo majumbani mwao,” alisema Sheikh
Nasoro.
Sheikh
Nasoro aliwataka Waislam mkoani hapa kusherehekea sikukuu hiyo kwa salama na Amani
huku akihimiza kuwalinda watoto na kuacha usalama kwenye nyumba zao watakapo
kuwa sehemu tofauti tofauti kusherehekea sikukuu hiyo kwani wezi nao wanatumia
nafasi hiyo kwenda kuiba.
Aidha,
Sheikh Nasoro aliwaomba wafanyabiashara kushusha bei ya vyakula na nguo wakati
huu wa sikukuu ili watu wasio na uwezo waweze kununua na kuwavika watoto hao
jambo ambalo litawafanya kupata fadhira ya Mwenyezi Mungu.
Sheikh Nasoro aliwataka Waislam mkoani hapa kutosherehekea sikukuu hiyo kwa kunywa pombe, kufanya ufusika na matendo mengine yasiyo mpendeza Mwenyezi Mungu bali wayaishi matendo yote mema waliyoyafanya wakati wa kipindi cha Mwezi Mtukufu wa Ramadhani.








No comments:
Post a Comment