MKAZI WA SINGIDA ALIYE ANGUKA KWENYE MTI AKILINA ASALI AOMBA MSAADA WA FEDHA ZA MATIBABU - SINGIDANIBLOG

Habari za Hivi Punde

Post Top Ad

Wednesday, April 9, 2025

MKAZI WA SINGIDA ALIYE ANGUKA KWENYE MTI AKILINA ASALI AOMBA MSAADA WA FEDHA ZA MATIBABU

Mkazi wa Kijiji cha Mkulu Wilaya ya Singida, Juma Mohamed Swalehe aliyechuchumaa, akiwa na katika picha ya pamoja na wenzake.

...............................................

Na Dotto Mwaibale, Dar es Salaam

MKAZI wa Kijiji cha Mkulu Wilaya ya Singida, Juma Mohamed Swalehe ambaye amelazwa Taasisi ya Mifupa Muhimbili (MOI)   jijini Dar es Salaam kwa matibabu baada ya kuanguka  kwenye mti alipokwa akilina asali Machi 27, 2025 anaomba msaada wa fedha za matibabu.

Hali ya mgonjwa huyo mwenye namba ya kupokelewa hospitalini hapo 4474017 na mwenye faili la matibabu namba 491432 imeelezwa bado siyo nzuri na bado anaendelea na matibabu kufuati uti wake wa mgongo kupata madhara.

Akizungumzia tukio hilo Sheikh Abtway Said Kumala ambaye pia ni Mratibu Mkuu wa Msikiti wa Ibn Abass  uliopo Kijiji cha Nduamghanga Mkulu Tarafa ya Mgori Kata ya Mghunga Wilaya ya Singida alisema baada ya kuanguka na kuwa katika hali mbaya alipelekwa Hospitali ya Makiungu iliyopo Wilaya ya Ikungi lakini kutokana na hali yake kuwa mbaya alipewa rufaa kwenda Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) ambako anaendelea na matibabu.

“Tumeambiwa kuwa hali yake imekuwa ikibadilika na kupelekwa mara kadhaa chumba cha wagonjwa mahututi lakini tunamshukuru Mwenyezi Mungu madaktari wanampambania,” alisema Sheikh Kumala.

Alisema changamoto kubwa iliyopo ni fedha za matibabu anazodaiwa ambapo awali alitakiwa kulipa Shilingi 900,000 ambazo walifanikiwa kuzitoa baada ya ndugu na jamaa kuchangishana lakini sasa imetoka bili mpya ambapo zinahitajika Sh.Milioni 2,314,780.00.

Amesema kutokana na bili hiyo na familia kutokuwa na uwezo wa kuilipa wanawaomba wananchi na na wadau mbalimbali kusaidia kupatikana kiasi hicho cha fedha kwa ajili ya mpendwa wao huyo aliyopo hospitalini ili aendelee kupatiwa matibabu kwani hawezi kusimama zaidi ya kulala wakati wote.

Kumala amesema kwa mtu yeyote atakaye kuwa tayari kumsaidia kada huyo wa CCM ambaye anaendelea kupata matibabu anaweza kuwasiliana naye kwa namba 0762606042 au namba 0782011608 ili kujua namna ya kupokea msaada huo.

Ndugu zangu watanzania shimeshime tujitokeze kumsaidia mwenzetu huyu kwa kutoa chochote tutakacho jaaliwa na Mwenyezi Mungu na tutabarikiwa kwa utoaji wetu.

Hii ndio bili ya fedha inayotakiwa kulipwa.
Sheikh Abtway Said Kumala ambaye pia ni Mratibu Mkuu wa Msikiti wa Ibn Abass  uliopo Kijiji cha Nduamghanga Mkulu Tarafa ya Mgori Kata ya Mghunga Wilaya ya Singida.
 

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad