Mtia nia wa ubunge Jimbo la Busokelo, Ezekiel Mwakyambo Gwatengile akionesha fomu ya kugombea nafasi hiyo baada ya kukabidhiwa Juni 28, 2025 katika ofisi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tukuyu wilayani Rungwe.
Na Dotto Mwaibale
MTAALAMU wa Masuala ya ugavi, ununuzi na masoko Ezekiel Mwakyambo Gwatengile tayari amechukua fomu ya kugombea Ubunge jimbo la Busokelo lililopo Rungwe mkoani Mbeya kupitia Chama Cha Mapinzuzi (CCM), ambapo atapambana na Mbunge aliyemaliza muda wake, Atupele Mwakibete anayetetea nafasi hiyo.
Wagombea wengine ambao wametajwa kuwania nafasi hiyo ni aliyekuwa mkuu wa mkoa mstaafu wa Kigoma, Thobias Andengenye,, Wakili Gerald Mwayonde na Lutengano Mwalwiba.
Gwatengile anauzoefu wa uongozi kwani amewahi kushiriki makongamano mbalimbali ya kitaifa na kimataifa, amewahi kuwa Mwenyekiti wa UVCCM Tawi, Mjumbe Mwakilishi wa CCM Wilaya, na sasa anahudumu kama Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Mkoa wa Mbeya hadi mwaka 2027. Pia ni Mwenyekiti wa BUDEA, KAMBADEA na UKUKIKAMA jijini Dar es Salaam, hivyo kuwa na mchango mkubwa katika ustawi wa jamii.
Katika jimbo hilo Serikali imefanya kazi kubwa chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kupitia mbunge aliyemaliza muda wake, Atupele Mwakibete, lakini kutokana na kuwepo kwa demokrasia watia nia hao wa nafasi hiyo wamejitokeza ili atayefanikiwa kuwa mbunge aweze kuendeleza maendeleo zaidi kwenye maeneo ambayo bado yana changamoto kwenye sekta ya elimu, afya, barabara, umeme, kilimo na mengineyo.
Jimbo la Busokelo linahitaji kupata viongozi wenye uwezo, maono na ubunifu ili liweze kupiga hatua kubwa ya maendeleo na kutekeleza kwa vitendo ilani ya uchaguzi ya 2025/ 20230.
Mtia nia huyo Gwatengile akijaza fomu hiyo baada ya kukabidhiwa.
Mtia nia huyo Gwatengile akikabidhiwa fomu hiyo.







No comments:
Post a Comment