Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia
Suluhu Hassan (katikati), akiwa pamoja na viongozi mbalimbali wakati wa Mkutano Maalum wa chama hicho uliofanyika ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete (JKCC)
Jijini Dodoma Mei 29,2025.
............................
Na Dotto Mwaibale
JANA Julai 25, 2025 Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (NEC), Itikadi na Mafunzo, Amos Makalla aliutangazia umma kupitia vyombo ya habari
kwamba chama hicho leo Julai 26, 2025 kitafanya mkutano mkuu maalumu kwa njia ya mtandao.
Mara baada ya tamko
hilo la Makalla kumekuwa na maneno mengi kutoka kwa baadhi ya wananchi wakihoji ni kwanini chama hicho kinafanya
mkutano kwa njia hiyo kwa sababu jambo hilo halijazoeleka.
Hata hivyo, kufanya mikutano kwa njia ya mtandao ni jambo ambalo limeanza siku nyingi duniani
na limekuwa likisaidia kupunguza gharama kwani kufanyika kwa mikutano wa njia
hiyo mtu anaweza kushiriki mkutao husika
akiwa eneo lolote alipo.
Lakini hoja ya baadhi ya
wananchi wanaona jambo hilo
ni kama limekiukwa na chama hicho kitu ambacho sio cha kweli kwani CCM
iliona mbali na ndio maana katika katiba yake iliyofanyiwa maboresho ilianisha
kuwa kunaweza kufanyika mikutano ya chama
kwa njia ya mtandao.
Ni kwa msingi huo
wanaohoji suala hilo kwamba kanuni
zimekiukwa hawana hoja na wanapaswa
kuisoma katiba ya chama hicho Toleo la Mei 2025 ibara ya 99 (i) na (ii) A - F inaeleza vikao
vilivyoorodheshwa kwenye (i) vinaweza kuendeshwa kwa njia ya Mtandao kama kuna
ulazima wa kufanya hivyo.
Vikao hivyo ni Mkutano
Mkuu wa CCM Taifa, Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu
ya CCM Taifa, Kamati Maalum ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Sekretarieti ya
Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Sekretarieti ya Kamati Maalum ya Halmashauri Kuu
ya CCM Taifa Zanzibar, Kamati ya Wabunge Wote wa CCM, Kamati ya Wajumbe wote wa
Baraza la Wawakilishi wa CCM Zanzibar.
Hatua hiyo ya CCM
kufanya mkutano huo kwa njia ya mtandao huenda imelenga kupunguza gharama na muda
ambao ungetumika hasa kwa kuzingatia chama kina mambo mengi ya kufanya ukiwepo
mchakato wa kupitisha majina ya watia nia waliomba ridhaa ya kuwania nafasi ya
udiwani na ubunge.
Makala alisema maandalizi ya mkutano huo utakaofanyika leo tayari yamekamilika na kuwa moja ya ajenda yake kuu ni kufanya marekebisho madogo kwenye katiba.









No comments:
Post a Comment