Nilikuwa nimejaribu mara mbili mtihani wa mwisho wa shahada yangu lakini nilishindwa.
Familia yangu ilianza kupoteza imani nami, na hata walimu wangu walinitazama kwa huruma kana kwamba nilikuwa kesi ya kupoteza muda. Wengine walinicheka wakisema ningebaki historia kama mwanafunzi aliyeshindwa kuhitimu licha ya miaka yote ya kusoma.
Kila mara nilipokumbuka machozi ya mama yangu na maneno ya baba yangu kuwa labda siyo kila mtu amezaliwa kusoma, moyo wangu ulijaa huzuni.
Nilijaribu kusoma usiku na mchana, nikafanya mazoezi ya maswali na hata kuhudhuria masomo ya ziada, lakini akili yangu haikunisaidia.
Nilihisi kama kulikuwa na nguvu fulani imenifunga, ikinivuta nyuma kila nilipojaribu kupiga hatua mbele.
0 Comments