SHEREHE KIPAIMARA YA WATOTO CATHERINE SKANA NA BENJAMIN MANASE YAJAA MAFUNDISHO - SINGIDANIBLOG

Habari za Hivi Punde

Post Top Ad

Sunday, November 30, 2025

SHEREHE KIPAIMARA YA WATOTO CATHERINE SKANA NA BENJAMIN MANASE YAJAA MAFUNDISHO

 

 Watoto Catherine Skana na Benjamin Manase ,wakikata keki maalumu kwa ajili ya sherehe yao ya kipaimara iliyofanyika nyumbani kwako Chang'ombe Mtaa wa Mazengo Novemba 30/ 2025 Jijini Dodoma.

...................................

Na Dotto Mwaibale, Dodoma.

SHEREHE ya Kipaimara cha watoto Catherine Skana na Benjamin Manase wa Chang'ombe Mtaa wa Mazengo Jijini Dodoma imekuwa ya aina yake kutokana na sehemu kubwa kujaa nasaha na kufundwa  huku wakielezwa kuwa nasaha hizo zitawasaidia katika maisha yao.

Sherehe hiyo ilifanyika baada ya ibada ya sakramenti ya ubatizo na kipaimara iliyofanyika Kanisa la Moravian Tanzania Jimbo la Kaskazini Usharika wa Nkuhungu Jijini Dodoma ambayo iliongozwa na Mchungaji wa Usharika huo Ephraim Mbise na  muhubiri wa neno la Mungu alikuwa ni Mchungaji Ester Mwasyoge ambaye ni Mwenyekiti wa wilaya wa kanisa hilo katika jimbo hilo Dodoma. 

Salome Daniel ni mama mlezi wa watoto hao ambaye alitumia nafasi hiyo kuwasihi kuendelea kukua katika maadili mema kama ambavyo wamekuwa wakielekezwa wakati wote.

“Babu na Bibi yenu Mzee Hebron Mwaibale ambao wametangulia mbele ya haki tuliishi nao vizuri na walikuwa wakiwalea wazazi wenu katika misingi mizuri ya upendo, kumuheshimu kila mtu na ndiyo maana na sisi tumeendelea kuwa  nanyi na tuna wasisitiza mufuate nyayo zao,” alisema Daniel.

Daniel alisema wamehudhuria sherehe hiyo kutokana na ushirikiano mzuri uliojengwa na babu na bibi yao ambao walikuwa ni rafiki wa kila mmoja katika mtaa huo wa Mazengo.

Mama Amina ambaye ni jirani wa watoto hao aliwaomba watoto hao waendelee kushikamana kama walivyo wazazi wao na kuwa hiyo ndiyo silaha pekee ya kujilinda na mtu yeyote watakao muona anataka kuwatenganisha.

“Endelea kushirikiana na watoto wenzetu wa mtaa huu katika masomo, kuwasaidia wazazi wenu kufanya kazi mbalimbali na kumheshimu kila mtu, pasipo kusahau kusali jambo litakalowasaidia kufika mbali kimaisha,” alisema Mama Amina.

Katika sherehe hiyo iliyohudhuriwa na mamia ya watu kulikuwa na burudani mbalimbali ambazo ziliongonzwa na Mshereheshaji maarufu wa eneo hilo MC Mwajuma Nassoro  na kusindikizwa na nyimbo za kabila la wanyakyusa na Kigogo pamoja na msosi wa nguvu ulioandaliwa na wazazi  wa watoto hao kwa kushirikiana na majirani.Watoto Catherine Skana na Benjamin wakilishana keki katika sherehe hiyo.Watoto Catherine Skana na Benjamin wakiwa wamepozi kwenye sherehe hiyo.Watoto hao wakituzwa zawadi.

Kutuzwa zawadi kukiendelea.
Catheline na Benjamin wakiwa na watoto wenzao kwenye sherehe hiyo.
Watoto wenzao nao wakijumuika kupata keki.
Catherine akilisha keko mama yake Bumi Heblon Mwaibale.
Benjamin akijiandaa kumlisha keki mama yake Bumi Mwaibale.
Mjomba Lusajo Mwaibale akilishwa keki. "Ni kama anasema keki tamu hii balaa"
Mama walezi wa watoto hao wakilishwa keki.
Mama wa watoto hao Lilian Hebron Mwaibale akijiandaa kulishwa keki.
Wageni waalikwa na ndugu, jamaa na marafiki wakijumuika pamoja kuserebuka.
Mserebuko ukiendelea.
Hapa ni sura zenye furaha tupu wakati wa sherehe hiyo.
Ni furaha tupu kwenye sherehe hiyo.
Catherine na Benjanin wakielekea eneo lililoandaliwa kwa sherehe hiyo.
Sherehe ikinogeshwa na vazi maalumu.
Sherehe ikiendelea.
Sherehe ikiendelea. Wageni waalikwa wakijumuika na familia ya Hebron Mwaibale kwenye sherehe hiyo.
Watoto wakiwa kwenye sherehe hiyo
Mjomba wa watoto hao Lusajo Hebron Mwaibale akiwapa zawadi wajomba zake.
Mama wa watoto hao Bumi Mwaibale (kulia) akiserebuka na rafiki zake katika sherehe hiyo.
Watoto wakipongezwa na kutunzwa mizawadi.

Watoto hao wakitunzwa zawadi
Mama wa watoto hao Bumi Mwaibale, akitunzwa.
Mama wa watoto hao Lilian Hebron Mwaibale akitunzwa na rafiki zake.
Chakula kikigawiwa.
Chakula kikiandaliwa.
Wakati wa chakula.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad